Wednesday, April 3, 2013

RAIS KIKWETE AELEZA ALIVYOOMBEWA DUA NA WAISLAMU ILI AFE.....

                                                Rais Jakaya Mrisho Kikwete.
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete ‘JK’ amelilipua kundi dogo la Waislam waliowahi kumsomea Itikafu ili yeye na viongozi wawili wa serikali wafe kwa kile kilichodaiwa na kundi hilo kwamba, wamekuwa wakiiangamiza dini yao.

Hayo yalisemwa na JK mwenyewe katika hotuba aliyoitoa ikulu Machi 31, 2013 ambayo ni utaratibu aliojiwekea wa kuwahutubia Watanzania kila mwisho wa mwezi.

JK alikuwa akijibu tuhuma zinazoelekezwa kwake kutoka pande zote za dini ya Kiislam na Kikristo kwamba amekuwa akipendelea upande mwingine.

Akizungumza bila kumung’unya maneno lakini katika hali iliyoonesha kusikitishwa na madai hayo, JK alisema:
“Ndugu wananchi, nyaraka na kauli kalikali zinazotolewa na viongozi wa dini za Kikristo na Kiislam zinanishawishi kuamini haya niyasemayo. Nyaraka na kauli hizo zina mambo mawili makuu.

KAULI YA UCHUNGU ALIYOTOA ABSALOM KIBANDA BAADA YA KUTEKWA NA KUTOBOLEWA JICHO

        Kauli  hii  ameitoa  kupitia  ukurasa  wake  wa  facebook:

Si jambo rahisi kibinadamu ingawa kwa Mungu hakuna lisilowezekana. Japo miye ndiye mwenye maumivu makali na machungu mwilini yanayotokana na majeraha na ulemavu niliotiwa, mke wangu kipenzi al maarufu Mama Joshua alikuwa pembeni mwangu wakati wote nikiwa kitandani hospitalini Dar es Salaam hadi Milipark Afrika Kusini. Pole sana Angela.

Matendo yanasema zaidi kuliko maneno...umepita nyakati nyingi sana ngumu juu yangu tangu mwaka 2000 tulipokutana na kuwa marafiki na hatimaye mwili mmoja.

Ni Mungu tu atakayekulipa kile kinachostahili na si mwanadam

Magazeti ya leo Jumatano ya 3rd April 2013




KAJALA MASANJA AJICHORA TATTOO YA WEMA SEPETU MGONGONI KAMA ISHARA YA KUMSHUKURU KWA ZILE MILIONI 13

Kajala ameamua kuchora Tattoo yenye jina la WEMA mgongoni mwake  baada ya kutolewa faini ya Shilingi Milioni 13 na msanii mwenzake Wema Sepetu,

hii ikiwa kama ishara ya shukrani kwa rafiki yake kipenzi Wema Sepetu.

WAZIRI MKUU AHUDHURIA MISA YA PAMOJA JIJINI ARUSHA YA KUAGA MAREHEMU WALIOFUKIWA NA KIFUSI

                                       Sehemu ya majeneza ya marehemu katika ibada hiyo maalumu leo

 Mh Waziri Mkuu Mizengo Pinda akitia saini kitabu cha maombolezo alipofika mkoani Arusha leo Kuwapa pole ndugu na jamaa ambao ndugu zao wamefariki katika machimbo ya Moramu katika eneo la Moshono Mkoani Arusha. Maporomoko hayo yametokea jana na kusababisha vifo vya watu13 na majeruhi wawili ambao mmoja ameruhusiwa na mwingine amelazwa katika Hospitali ya Mount Meru

LADY JAYDEE AAMUA KUFUNGUA KITUO CHAKE CHA REDIO BAADA YA KUCHOSHWA NA MANYANYASO YA CLOUDS FM

Hatimaye tumepata jibu la kwanini Judith Mbibo aka Lady Jaydee amekuwa akitweet vitu vizito weekend iliyopita. Kama hukufaniwa kuziona tweets hizo ni kwamba mwanadada huyo alishusha mfululizo wa mabomu kuelekea kwa kituo kimoja cha radio na kujikuta akiongeza aka mpya, Anaconda.

Na sasa imebainikiwa kuwa mwanamuziki huyo mkongwe na mjasiriamali anakuja na kituo chake cha radio kiitwacho Kwanza FM. Habari hiyo aliibreak mwenyewe jana na bila shaka haihusiani na April’s Fools Day.

    Kwanza FM coming soon. Yangu mwenyewee