Monday, February 2, 2015

Bondia Francis Cheka amehukumiwa kwenda jela.

Bondia Francis Cheka leo February 2 2015 amehukumiwa kwenda jela miaka mitatu na faini ya Milioni moja laki sita kwa kosa la kumpiga mmoja kati ya wafanyakazi wake kwenye bar yake iliyopo Morogoro.

Muda mfupi uliopita Francis Cheka ameongea  na kusema ndio alikua anajiandaa kuachia simu yake na vitu vingine muhimu ili achukue karandinga kuelekea gerezani ambapo namnukuu akisema ‘imeshakua hivi tayari ila hamna noma, niko na wanangu wengine wamepigwa miaka 10 nitakua nao fresh tu ila hamna noma ni miaka mitatu tu mimi’

Hukumu imetolewa na Hakimu Mkazi Said Msuya ambapo baada ya hayo upande wa Francis Cheka unasemekana kujiandaa kukata rufaa.

millardayo.com

Habari njema kuhusiana na majaribio chanjo ya Ebola…


Stori kuhusu ishu ya Ebola huenda ni moja ya story zilizochukua headlines kubwa kwa mwaka wote 2014, tangu iliporipotiwa kuibuka kwa maambukizi ya ugonjwa huo Afrika Magharibi mwanzo wa mwaka 2014.

Hii inaweza kuwa habari njema kwa Waafrika na dunia nzima kwa ujumla, taarifa iliyopo ni kwamba jaribio la kwanza la chanjo ya ugonjwa wa Ebola kutarajiwa kuanza kutumika Liberia wakati wowote kuanzia sasa.

Wataalamu wanatarajia zaidi ya watu 30,000 watajitokeza katika zoezi la majaribio hayo wakiwemo wahudumu wa afya.

Katika kipindi cha mwaka mmoja zaidi ya watu elfu tisini wamefariki kutokana na ugonjwa huo ambao uliandama zaidi Mataifa ya Guinea, Sierra Leone na Liberia.

Toto langu kazini chezea precious wewee