Saturday, January 5, 2013

Mama Bilal Mgeni Rasmi Tambaza

 Mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Asha Bilal, akisoma hotuba yake wakati alipokuwa mgeni rasmi kwenye Mahafali ya Kidato cha Sita kwa Jumuiya ya Wanafunzi wa Kiislamu wa Shule ya Sekondari ya Tambaza. Mahafali hayo yamefanyika leo Januari 05, 2013 katika shule hiyo ya Tambaza jijini Dar es Salaam. Katika hotuba yake Mama Asha amewahasa vijana hususan wanafunzi hao waliohitimu masomo kutokukubali kutumika na watu wenye maslahi binafsi na kujikuta wakisababisha uvunjifu wa amani. Aidha amewataka kutojihusisha na makundi yanayochochea uvunjifu wa amani bila kujitambua wafanyalo, badala yake amewaomba kuwa wakipima kila wanaloambiwa kuwa linamaslahi na dini yao ama maslahi kwa jamii na taifa kwa ujumla.

Mke wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Asha Bilal, akimkabidhi zawadi mhitimu wa Kidato cha Sita, Zuhura Azmin, kwa kuwa mmoja kati ya waliofanikisha sherehe za mahafali ya Kidato cha Sita kwa Jumuiya ya Wanafunzi wa Kiislamu wa Shule ya Sekondari ya Tambaza

Waziri Membe atangaza kutogombea Ubunge tena

                Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe.

Membe ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Mtama, mkoani Lindi, alitoa kauli hiyo alipokuwa akizungumza kwenye sherehe za Mwaka Mpya nyumbani kwake.

WAZIRI wa Mambo ya Nje na ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe ametangaza kuwa hatogomea tena ubunge katika uchaguzi mkuu ujao.

Membe ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Mtama, mkoani Lindi, alitoa kauli hiyo alipokuwa akizungumza kwenye sherehe za Mwaka Mpya nyumbani kwake.

“Unajua nimekuwa mbunge wenu kwa kipindi cha tatu. Hivi leo ninawaaga rasmi kuwa sitagombea tena nafsi hii ya ubunge,” alisema Membe.

kinana akemea chokochoko za kidini

KATIBU Mkuu wa CCM,Abdulrahman Kinana amekerwa na chokochoko za kidini zilizoanza kujipenyeza hivi karibuhi na kutoa wito kwa madhehebu ya dini na taasisi zake hapa nchini,kuendelea kuhubiri amani kwa kuliombea taifa , ili wananchi waendelee kujivunia amani iliyoachwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere.

Kinana alitoa kauli hiyo juzi kwenye maadhimisho ya siku ya kumbukumbu ya Imam Husein, yanayoadhimishwa na dhehebu la KhojaShia Ithna Asheri Jamaat Arusha kote duniani na kufanyika kwenye msikiti wa jumuiya hiyo jijini hapa , ambapo watu mbalimbali wakiwamo viongozi wa madhehemu pamoja na viongozi wa chama na Serikali walihudhuria.

Kinana alisema kuwa upo umuhimu mkubwa kwa viongozi wa dini na taasisi zake kuendelea kuienzi amani kwa kuhubiri suala la kudumisha amani na kuonya kwamba Serikali haitasita kuchukua hatua za haraka kwa mtu ama kikundi chochote cha dini kitakachojihusisha na uvunjivu wa amani.

NDEGE MEDICS YAKABIDHI AMBULANCE ZA KISASA

 Head of Primary Medical Centre Bwa. Siwawi Konteh (wa pili kulia) ambaye pia ni mratibu wa mradi wa Tuunganishe Mikono Pamoja ili kuokoa Afya ya Mama na Mtoto akizungumzia Malengo Makuu ya mradi huo kuwa ni kuongeza kiwango na matumizi ya Huduma ya Afya ya Mama Mjamzito na Watoto na kushirikiana na kujifunza kuhusu Afya ya Mama Mjamzito na Mtoto. Kutoka kushoto ni Acting Medical Director wa Aga Khan Hospital Dr. Ambrose Chanji, Mwenyekiti wa Bodi ya Hospitali ya Aga Khan Bw. Amin Habib, Mkurugenzi Mkuu na Mwenyekiti wa Ndege Medics Dr. Sebastian Ndege na Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Rasilimali Watu cha Hospitali hiyo Bw. Anis Nazrani.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Hospitali ya Aga Khan Bw. Amin Habib (kushoto) na Mkurugenzi Mkuu na Mwenyekiti wa Ndege Medics Services Limited Dr. Sebastian Ndege wakikata utepe kuashiria kukabidhiwa magari ya kubeba wagonjwa kwa Hospitali ya Aga Khan ikiwa ni katika mradi wa kuboresha Afya ya Mama Mjamzito na Mtoto Tanzania
                                Wakipongezana baada ya makabidhiano hayo.
 Pichani Juu na Chini ni muonekano wa magari hayo ya kubebea wagonjwa kwa ndani yaliyotelwa kwa hospitali ya Aga Khan na NDEGE Medics kwa ajili ya mradi wa kuboresha Afya ya Mama Mjamzito na Mtoto Tanzania.

walionunua ving'amuzi star times waambiwa wavirejeshe

KAMPUNI ya Star Media Tanzania Ltd (Startime) imewataka watu ambao wamenunua ving’amuzi na kubaini kuwa havifanyi kazi kuvirejesha kwenye ofisi zao ili wapatiwe vingine.
Vilevile wamewataka wale waliouziwa kwa bei ya kulangua wafike kwenye ofisi zao pamoja na risiti walizonunulia ili hatua zinazofaa ziweze kuchukuliwa.

Hatua hiyo inatokanana malalamiko ya wananchi siku chache tangu kuanza kutumika kwa mfumo wa dijitali wa kurusha matangazo ya runiga.

Malalamiko hayo yanayolalamikiwa na kampuni hiyo ni kuhusiana na kushindwa kuonekana kwa baadhi ya chaneli licha kufunga king’amuzi kwenye Televisheni

Waziri Membe atangaza kutogombea ubunge tena

WAZIRI wa Mambo ya Nje na ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe ametangaza kuwa hatogomea tena ubunge katika uchaguzi mkuu ujao.Membe ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Mtama, mkoani Lindi, alitoa kauli hiyo alipokuwa akizungumza kwenye sherehe za Mwaka Mpya nyumbani kwake.

“Unajua nimekuwa mbunge wenu kwa kipindi cha tatu. Hivi leo ninawaaga rasmi kuwa sitagombea tena nafsi hii ya ubunge,” alisema Membe.

, ambapo pia aliwataka wananchi wa mikoa ya kusini, kuwa na subira katika kipindi hiki ambapo Serikali inashughulikia mchakato wa kuvuna gesi asilia.

Leo ikiwa ni siku ya kuwakumbuka Denis na Ismail chadema yafanya shughuli za kijamii...

 Moja ya vituo vya kulelea watoto yatima alivyo vitembelea Godbless Lema na katibu mkoa Amani
 Mh. Lema akiwa na watoto yatima kati ya vituo alivyotembelea leo katika siku ya kuwakumbuka Denis na Ismil.
 Huyu mtoto YATIMA ameshika nafasi ya tatu ktk Wilaya Arusha matokeo ya la saba..
CHADEMA Arusha leo itakuwa na Kumbukumbu ya miaka miwili (2) ya mauaji ya makusudi ya raia wasio kuwa na hatia yaliyotokea 5/1/2011.Kumbukumbu hii itaenda sambamba na chama kufanya shughuli za kijamii,ikiwepo kutembelea vituo vitano vya watoto yatima jijini Arusha,kutoa wafungwa waliofungwa kwa kukosa faini ya ela ndogo,kisha kuhitimishwa kwa mkutano mkubwa wa hadhara.

Tunaomba wapenda haki wote kujitokeza kwa wingi siku ya Jumamosi 5/1/2013 katika ofisi za chama Ngarenaro,kwa ajili ya kwenda kutoa misaada hiyo kwenye vituo vya Yatima,pia tunatoa wito kwa kila mmoja wetu kujitolea chochote anachoweza Sukari/mchele/sabuni/mafuta etc kama ishara ya kutoa Sadaka,kwa Mwenyenzi Mungu ili HAKI iweze kutendeka.

Tutaendelea kudai haki na usawa katika jamii yetu hata kwa gharama ya maisha yetu.Denis na Ismail pamoja na wengine wengi tutawakumbuka daima,damu yenu hakimwagika bure,

Mwanajeshi Aliyepiga Picha na Mbunge wa Arusha Mjini-Chadema Godbless Lema Kwenye Mkutano wa Hadhara Akamatwa


 Mtu aliyejitambulisha kuwa askari wa Jeshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ),kambi ya Monduli,Arusha kwenye mkutano wa Chadema Mji mdogo Mererani,Simanjiro mkoani Manyara hivi karibuni akiwa ndani ya gari ya jeshi baada ya kutiwa nguvuni,
 Mtu aliyejitambulisha kuwa askari wa Jeshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ),kambi ya Monduli,Arusha akiwa na wabunge wa Chadema, Godbless Lema (Arusha Mjini) na Joshua Nassari (Arumeru Mashariki) baada ya kumalizika kwa mkutano wa hadhara uliohutubiwa na wabunge hao katika Mji mdogo Mererani,Simanjiro mkoani Manyara hivi karibuni.
 Picha juu alipopiga picha na Viongozi mbalimbali wa Chadema Mtu aliyejitambulisha kuwa askari wa Jeshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ),kambi ya Monduli,Arusha akiwa na wabunge wa Chadema, Godbless Lema (Arusha Mjini) na Joshua Nassari (Arumeru Mashariki) baada ya kumalizika kwa mkutano wa hadhara uliohutubiwa na wabunge hao katika Mji mdogo Mererani,Simanjiro mkoani Manyara hivi...
                                                 

Magazeti ya leo Jumamosi ya 5th January 2013




Leo Chadema Wawakumbuka waliopoteza Maisha katika vurugu zilizotokea 5/1/2011 Arusha.

Kwa wakazi wa Arusha na vitongoji vyake, Leo kutakuwa na mkutano mkubwa wa kuwakumbuka ndg zetu(Denis na Ismail) walio pigwa risasi na jeshi la polisi 5.1.2011, mkutano huu utafanyika kwenye uwanja wa Ngarenaro shule ya msingi kuanzia saa tisa, vile vile utarusha na kituo cha redio ya sunrise (94.80 FM) kwa wakazi wa Arusha na mikoa jirani.






Hizi ni baadhi ya picha wakati wa kuwaaga makamanda wetu waliopoteza maisha 5.01.2011. R.I.P (Denis na Ismail)