Friday, May 31, 2013

TAARIFA YA UCHUGUZI JUU YA KUTEKWA NA KUUMIZWA KWA ABSALOM KIBANDA HII HAPA

Mhariri Mtendaji wa New Habari (2006) Ltd na Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Absalom Kibanda

TAARIFA YA UCHUGUZI JUU YA KUTEKWA NA KUUMIZWA KWA ABSALOM KIBANDA IMEWASILISHWA NYUMBANI HOTEL – TANGA MEI 30, 2013

UTANGULIZI:Usiku wa Jumanne ya Machi 5 kuamkia Machi 6, 2013, Mhariri Mtendaji wa New Habari (2006) Ltd, ambaye pia Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Absalom Kibanda alivamiwa na kujeruhiwa vibaya akiwa nje ya lango la kuingilia nyumbani kwake Mbezi Juu, Dar es Salaam.

Tukio hilo liliishtua na kutikisa taifa kwa kiwango kikubwa si tu katika tasnia ya habari nchini, bali pia jamii kwa ujumla hasa baada ya aina ya utekaji, utesaji na usiri uliotumika katika kufanikisha uhalifu huu kufanana kwa karibu na tukio lilomkuta Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madkatari Tanzania, Dk. Stephen Ulimboka lililotokea karibu miezi tisa kabla ya tukio la Kibanda yaani, usiku wa Juni 26, 2012.

RASIMU YA KATIBA MPYA YAPENDEKEZA KUWEPO KWA SERIKALI TATU.....

Leo ni ufunguzi wa rasimu  ya katiba  mpya  na Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba amesema  kwamba  Rasimu hiyo  imependekeza kwamba matokeo ya rais yahojiwe mahakamani.

Kwa lugha nyingine ni kwamba katiba ijayo itaruhusu Rais kushtakiwa mahakamani endapo matokeo yake yatatiliwa shaka na wagombea wengine.

Jaji Warioba ameyasema hayo  wakati wa uzinduzi wa Rasimu ya Katiba Mpya katika tukio la kihistoria nchini Tanzania.

"Imependekezwa kwamba matokeo ya Rais yatashikiwa mahakamani lakini kwa masharti," amesema Jaji Warioba hivi punde.

M TO THE P ANAENDELEA VIZURI NCHINI AFRIKA KUSINI

Msanii M To The P aliyepelekwa hospitali pamoja na marehemu Albert Mangwea, kwa sasa anaendelea vizuri na matibabu kama anavyoonekana kwenye picha katika hospitali ya Helen Joseph huko nchini Afrika ya Kusini. (Picha kwa hisani ya Clouds FM)

Thursday, May 30, 2013

MZUMBE SECONDARY YAFUNGWA...WANAFUNZI WAPEWA SIKU MBILI WAPOTEE KATIKA MAZINGIRA YA SHULE

Wananfunzi wakidato cha kwanza hadi cha sita katika shule ya sekondari Mzumbe Morogoro wamelazimika kuandamana kwenda ofisi ya mkuu wa mkoa wa huo wakishinikiza kuboreshewa huduma muhimu.

Maboresha wanayodai kuboreshewa shuleni hapo ni pamoja na miundombinu, kuondoa ubadhirifu, uongozi mbovu na kukomeshwa vitendo vya lugha chafu zinazo tolewa na baadhi ya walimu.

Maandamano hayo yalizimwa mapema asubuhi baada ya jeshi la polisi kulazimika kufika katika eneo la
sangasanga barabara kuu ya Iringa Morogoro ambapo maandamano hayo yalikuwa yamefika kuelekea katika ofisi ya mkuu wa mkoa wa Morogoro.

Wananfunzi hawa wa shule ya sekondari Mzumbe Morogoro ya wenye vipaji maalum wanadai kuwa maandamano hayo yanatokea baada ya kuvumilia kwa muda mrefu na hivyo wameamua kupaza sauti zao wakibainisha matatizo lukuki yanayo wasibu ambayo yanaweza kushusha kiwango cha taaluma yao.

MAANDALIZI YA MSIBA WA NGWEA YAANZA MBEZI JIJINI DAR



NAIBU SPIKA AAPA KUTOMWADHIBU MBUNGE YEYOTE KWA MADAI KWAMBA AMECHOKA KUITWA ZEZETA

Naibu Spika wa Bunge,Ndugu Job Ndugai amesema kuwa kuanzia sasa hatamwadhibu Mbunge yeyote anayeleta vurugu Bungeni kwakuwa amechoka lawama.

 Akihojiwa na Redio One Stereo katika kipindi cha Kumepambazuka leo asubuhi ,Ndugai amesema kuwa yeye amechoka kuitwa mzembe,zezeta na goigoi na vyombo vya habari.

Ndugai amesema kuwa hata kwa Wabunge waliosababisha tafrani Bungeni jana kiasi cha kuchana Nyaraka za Bunge,hawatachukuliwa hatua yoyote.

TAARIFA YA MATOKEO MAPYA YA KIDATO CHA NNE, UFAULU WAPANDA KWA ASILIMIA 23....YAANGALIE HAPA.

                                   Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa.

Baraza la mitihani Tanzania NECTA limetangaza rasmi matokeo ya Kidato cha Nne 2012. Idadi ya watahiniwa waliofaulu mtihani wa kidato cha nne mwaka jana imeongezeka kwa kati ya asilimia 20 na 23 baada ya Baraza la Mitihani la Taifa (Necta), kufanya marekebisho alama za viwango vya ufaulu.

Matokeo hayo mapya yanaonyesha kuwa, ufaulu wa kuanzia daraja la kwanza hadi la nne umeongezeka kutoka asilimia 34.5 kwa matokeo yaliyotangazwa awali na huenda yakafikia asilimia 57.

Hii inamaanisha kwamba watahiniwa wapatao 82,000 ambao awali walikuwa wamepata sifuri katika matokeo ya awali sasa wamepanda na kupata madaraja ya ufaulu katika matokeo mapya.

P- FUNK AWACHANA TENA CLOUDS FM.... AELEZA JINSI MAREHEMU NGWEA ALIVYOGEUZWA NG'OMBE WA MAZIWA

Kwa mara nyingine  tena P-Funk amezungumzia sababu anazodhani zilipelekea marehemu Ngwea kujiingiza kwenye madawa.

Producer huyo ameichana CloudsFM kwa kile anachokiona kama unyanyasaji kwa wasanii, na kwamba dhuluma za Clouds Fm ni moja wapo ya vitu vilivyosababisha maisha ya Ngwear yawe na muelekeo mbaya.

 “Ngwair alikua kama ng’ombe wenu; mnamkamua tu maziwa.”  P funk

Akizungumzia kuhusu kuikataza Clouds FM kupiga nyimbo za Bongo Records  zikiwemo wa Ngwea, P-Funk amesema:

“Niko kwenye harakati za kuandaa barua ili nistopishe nyimbo zangu zote za Bongo Records, zisipigwe Clouds Fm.
Sababu kubwa ni uonevu wa haki miliki. Eti mnajiita  number one radio station??. Mnajidaganya .Kisaikolojia wasanii wote mmewateka.

Wote wanaona “bila kupeleka nyimbo zao Clouds hawatafanikiwa.” Mimi cha kwanza nataka kuonyesha mfumo mwingie kwamba bila nyinyi tutaweza. Cha pili mnaingiza hela sana ya wadhamini  lakini hamui-distribute kwa wanaohusika...
"Mfumo wa kupeleka nyimbo Clouds nilianzisha mimi . Hivyo nitakua wa kwanza kujitoa na kuanzisha mfumo mwingine.””

Wednesday, May 29, 2013

Yaliyojiri leo Jumatano Magazetini 29th May 2013





"SITAKI KUSIKIA NYIMBO ZA NGWEA ZIKIPIGWA CLOUDS FM..WAO NDO WALIOMFANYA AANZE KUVUTA BANGI ILI KUONDOA MAWAZO"...P FUNK

 Muda mfupi uliopita djchoka amepokea simu kutoka kwa Producer mkongwe hapa bongo anayejulikana kwa jina la P Fuck Majani na kumuuomba aipokee msg hii hapa chini na kuwaomba watanzania walijue hili na baadae atatoa barua rasmi.



KIFO CHA NGWEA: LADY JAYDEE NAYE ASITISHA SHOW YAKE

 Mwanamuziki nguli wa muziki wa kizazi kipya nchini, mwanadada Judith Wambura Maarufu kama Lady Jaydee ametangaza kuahirisha shughuli ya maadhimisho ya miaka 13 tangu aanze muziki iliyokuwa imapangwa kufanyika Ijumaa hii ya Mei 31, 2013 katika mgahawa wake wa Nyumbani Lounge kupisha msiba wa kifo cha msanii Albert Robert Mangweha aliyeripotiwa kufariki nchini Afrika Kusini jana.

Judith amesema hayo muda mfupi uliopita (saa 3:52 asubuhi) wakati akihojiwa katika kipindi cha Super Mix ya East Africa Radio na mtangazaji Zembwela.
 
Jaydee ameeeleza uamuzi wake wa kutitisha show hiyo kuwa unalenga kutoa nafasi kwa wafiwa wote na wadau wa tansnia ya muziki na wapenzi wa Mangwea kumaliza taratibu za kumsitiri kipenzi chao na kueleza kwamba tarehe nyingine ya shughuli hiyo itatangazwa baadae.

Tangu amekaribishwa studio, Judith Wambura alionekana kuwa na majonzi sana kiasi cha kushindwa kuongea mara kwa mara na kukatisha mazungumzo yake kutokana na kukabwa na kilio.

TAARIFA YA KIFAMILIA KUHUSU MAZISHI YA NGWEA NA JINSI MWILI HUO UTAKAVYOLETWA TANZANIA

Baba Mdogo wa Marehemu Mzee Mangweha ambaye yuko Mbinga Songea kikazi, amesema kuwa wamekubaliana na kaka yake mkubwa yaani baba mkubwa wa Ngwair, David Mangweha ambaye naye yuko Songea kuwa watu watakutanika Mbezi kwa msiba na pia mapokezi yatafanyika hapa Dar es salaam Mbezi Beach.
 
Ingawa bado kikao cha familia nzima hakijafanyika lakini baba huyo mdogo amesema wanaweza kulazimika kuzika Morogoro sehemu ambayo baba yake alizikwa.

Baba huyo mdogo alisema kuwa kesho ndo watarudi Dar es Salaam pamoja na kaka yake yaani baba mkubwa wa marehemu.

Kuhusu mwili kuletwa hapa Tanzania kutoka Afrika Kusini baba mdogo amesema kuwa mpaka sasa hawajajua jinsi gani mwili huo utafika hapa lakini kuna ndugu zao ambao tayari washaanza kufanya taratibu za kuwasiliana na ubalozi wa Afrika Kusini ili kujua ni jinsi gani mwili huo utafika hapa.

Kama kutakuwa na mabadiliko yeyote watakapowasili kesho baba mdogo na baba mkubwa baada ya kikao cha familia watatoa taarifa

Tuesday, May 28, 2013

BREAKING NEWS: ALBERT MANGWEA AFARIKI DUNIA....

Habari  zilizotufikia  ni  kwamba  msanii  Albert Mangwair  amefariki  dunia akiwa  Afrika  kusini

Chanzo  cha  kifo  hicho  bado  hakijafahamika  lakini  taarifa  za  awali  zinadai  kuwa  msanii  huyo  hakuamka  tangu  alipolala  jana.

Mtandao huu unaendelea  kuifuatilia  habari  hii 

R.I.P   Ngwair

"SINA SHAKA NA UMAARUFU WANGU"....LOWASSA

MBUNGE wa Monduli na Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa, amesema hana shaka na umaarufu wake Monduli wala Tanzania kwa ujumla.

Kauli hiyo aliitoa jana wakati akifungua kampeni za udiwani wa Kata ya Makuyuni huku akikishangaa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwa kupeleka mgombea wake katika Kata hiyo.

“Eti hawa wanathubutu kujinadi na kujigamba kushinda udiwani Monduli ya Lowassa wakisema watapata kura kwa asilimia 90 jamani haya ni kweli?,” alihoji Lowassa na kuongeza:

“Ndugu zangu sina shaka na umaarufu wangu Monduli wala Tanzania.”

Katika mkutano huo, aliwaambia wananchi kwamba anahitaji kuona wakikiadhibu CHADEMA kwa kukipa pigo ambalo hawajawahi kulipata mahali popote nchini.

KESI YA JAYDEE YARUSHWA MPAKA JUNE 13.

 Lady Jay Dee akiwa na mumewe Gardner Habash wakisuburi kesi kutajwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kindondoni

Mwanamuziki Judith Wambura-Habash --Lady Jay Dee-- alifika katika mahakama ya Kinondoni leo kama ilivyotakiwa kwa mashitaka aliyofunguliwa hapo. Baadaye amefahamisha kuwa ameambiwa arudi tarehe 13 Juni 2013.
Kesi imetajwa tena tar 13 June 2013. Saa 5 asub.

PENZI LA WASTARA LAGOMBANIWA.....

  TAKRIBAN  wiki moja baada ya kumaliza eda tangu alipofariki mumewe Juma Kilowoko ‘Sajuki’ Januari 2, mwaka huu, staa mkubwa wa filamu za Kibongo, Wastara Juma anagombewa na midume ikitaka kumuoa.

Akizungumza na mwandishi wetu  akiwa nchini Oman, Wastara alifunguka kuwa tangu amalize eda yake hiyo amekuwa akipata usumbufu mkubwa kutoka kwa wanaume mitandaoni na wanaomtamkia mwenyewe.

“Jamani mpaka nahisi kuchanganyikiwa kabisa, wanaume zaidi ya mia tano hata sijui walipotokea wanataka kunioa, hadi nahisi majanga,” alisema Wastara.

Wastara alisema kuwa wanaume hao wamekuwa wakihangaika bure kwa sababu kwa sasa hafikirii kabisa kuolewa kwani anapotembea bado anasikia harufu ya mumewe Sajuki.

“Bado harufu ya Sajuki ipo mwilini mwangu, wanaume wanaonitolea macho mtoto wa mwenzao wanakosea sana, sifikirii kabisa suala hilo kwa sasa,” alisema Wastara mwenye mtoto mdogo aliyezaa na Sajuki.

JACK WOLPER ALIA NA MATAPELI YANAYOTUMIA MITANDAO YA KIJAMII KWA JINA LAKE KUOMBA HELA WATU

Katika kile kinachoonekana ni mwendelezo wa matapeli wa mjini kutumia majina ya waigizaji maarufu nchini kutapeli watu kwa njia ya mtandao, dhahama hii sasa imemkuta mwanadada Jacqueline wolper baada ya watu wanaoaminika kuwa ni matapeli kutumia jina lake kujipatia fedha na vitu vingine kiudanganyifu.

Akizungumza kwa simu na tovuti ya bongomovies, mwanadada Jacqueline wolper  alisema matapeli hawa sasa wameamua kutumia mtandao wa instagram na mtandao mwingine wa kijamii uitwao badoo kwa jina la “wolper gambe25” katika kutapeli watu kwa kuwaomba hela au michango mbalimbali kupitia account hizo feki

“Leo nilikuwa naenda saluni, baada ya kufika tuu, yule dada wa saluni akaanza kunilalamikia kuwa mbona sijaenda kuchukua viatu nilivyomuagiza pamoja na hela?

NEEMA KWA WALIOFELI KIDATO CHA NNE....UFAULU WAONGEZEKA, MATOKEO NI MUDA WOWOTE

Idadi ya watahiniwa waliofaulu mtihani wa kidato cha nne mwaka jana imeongezeka kwa kati ya asilimia 20 na 23 baada ya Baraza la Mitihani la Taifa (Necta), kufanya marekebisho alama za viwango vya ufaulu, Mwananchi limebaini.

Habari ambazo gazeti hili imezipata zinasema matokeo hayo ambayo yamewezesha kiwango cha ufaulu kupanda na kufikia asilimia kati ya 54 na 57, huenda yakatangazwa wiki hii pamoja na yale ya kidato cha sita ambayo pia yamechelewa kutangazwa.

Chanzo cha habari kutoka Necta kimesema matokeo hayo mapya yanaonyesha kuwa, ufaulu wa kuanzia daraja la kwanza hadi la nne umeongezeka kutoka asilimia 34.5 kwa matokeo yaliyotangazwa awali na huenda yakafikia asilimia 57. Hii inamaanisha kwamba watahiniwa wapatao 82,000 ambao awali walikuwa wamepata sifuri katika matokeo ya awali sasa wamepanda na kupata madaraja ya ufaulu katika matokeo mapya.

Kwa matokeo hayo, watahiniwa wa mwaka 2012 watakuwa wamefanya vizuri kuliko wa mwaka 2011, ambao watahiniwa 225,126 sawa na asilimia 53.37 ya 349,390 waliofanya mtihani huo walifaulu.

Saturday, May 25, 2013

Magazeti ya leo Jumamosi 25th May 2013




WAASI WA M23 WATISHIA KUTUVAMIA MUDA WOWOTE....SERIKALI YA MKOA WA KAGERA YATOA TAHADHARI KWA WANANCHI

Serikali ya Mkoa wa Kagera imewatahadharisha wananchi wake kuepukana na wageni wasiowafahamu kwenye maeneo yao kutokana na tishio la kikosi chaM 23 cha nchini Congo DRC kinachotishia kuivamia Tanzania...
Kumekuwa na mapigano  makali  kati  ya waasi wa M23  na  vikosi vya serikali  nchini  Congo ambako jeshi letu lipo huko...

Waasi  hao  wametishia  kuivamia  Tanzania  muda  wowote  ili  kulipiza  kisasi.Miongoni mwa mipaka ambayo iko wazi  ni Kagera, na hii ndo sababu iliyopelekea  serikali ya Mkoa huo kutoa tahadhari kwa wananchi wake na watanzania kwa ujumla....

Credit: ITV

HUYU NDO MREMBO ATAKAYEWAKILISHA SHINDANO LA BIG BROTHER MWAKA HUU

                                                                 feza-kessy
                                                       feza-kessy-rick-ross-vanessa-mdee

Kwa mujibu wa ripoti kutoka kwenye   mitandao  mbalimbali nchini Tanzania, mrembo huyu, mwanamuziki Feza Kessy, ndiye atakayeiwakilisha Tanzania katika Big Brother Africa 2013 (BBA “The Chase.” Well, hizi ni baadhi ya picha zake.

Friday, May 24, 2013

TANZANIA,KENYA ZAVUTANA JUU YA VIJANA WALIOUWAWA NAROK

                                            Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Liberatus Sabas

MIILI  mitatu ya watanzania wa jamii ya Kisonjo waliouwawa katika eneo la Narok wilayani Kajiado nchini Kenya imeingia katika sura mpya mara baada ya Serikali ya Tanzania kushindwa kuirejesha nchini miili hiyo huku serikali ya Kenya ikidai kuwa hawakuwa watanzania

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Liberatus Sabas alisema kuwa tayari mtu mmoja ambaye ni askari polisi anashikiliwa na jeshi hilo kwa uchunguzi zaidi ingawaje alisema kwa sasa jina la askari huyo linahifadhiwa kwa ajili ya  upelelezi

Sabas alisema kuwa wanamshikilia askari huyo kwa kosa la upotevu wa silaha ambayo inasadikiwa kuwa ilitumika katika tukio uhalifu linalohusishwa na mauji ya vijana hao watatu wa Kitanzania nchini Kenya.

Kuhusu Marehemu hao, kamanda amesema kuwa Serikali ya Kenya kupitia Jeshi lake la polisi ndio wanajukumu la kurejesha  Miili yao hapa nchini .

Magazeti ya leo Ijumaa 24th May 2013




Flaviata Matata atoa wito kwa serikali kuhusu ajali ya MV Bukoba

Miss Universe Flaviana Matata akiwa na Mkurugenzi wa Compass communicayion, Maria Sarungi wakiwasha mshumaa kwenye kaburi la Marehemu mama yake mzazi aliyefariki katika ajali ya MV Bukoba mwaka 1996.

MWANAMITINDO wa kimataifa wa Tanzania, Flaviana Matata ameiomba serikali kutangaza Mei 21 ya kila mwaka kuwa siku maalum ya maombolezo ya wasiku maalum ya maombolezo ya wahanga wa MV Bukoba.
Ajali ya MV Bukoba ilitokea Mei 21 mwaka 1996 na kuua watu zaidi ya 1,000 na serikali kutangaza siku tatu za maombolezo ya kutokana na kuzama kwa meli hiyo iliyotokea kwenye Ziwa Victoria. Katika ajali hiyo, Flaviana alipoteza mama na kaka yake.

Flaviana ambaye kwa sasa anafanya shughuli za kuonyesha mitindo nchini Marekani na Uingereza, amekuwa mstari wa mbele kuadhimisha siku hiyo kwa kupitia taasisi yake ya Flaviana Matata Foundation.

Akizungumza Kwa niaba ya Flaviana Matata Mkurugenzi wa Compass Communications Company Limited Maria Sarungi Tsehai alisema pamoja na ajali hiyo kuua watu wengi, lakini inasikitisha kuona jambo hilo kwa sasa limekuwa kama kumbukumbu kwa wahanga wa ajali hiyo tu na si vinginevyo.
Maria ambaye alisema hayo katika misa maalum ya kumbukumbu ya ajali hiyo iliyofanyika kwenye makabuli ya Igoma, Mwanza alisema kuwa wakati umefika sasa wa kutangaza siku ya kitaifa ya maombolezo na kwani ajali hiyo imeacha Watanzania wakiwa na huzuni kubwa.

Alisema kuwa wanashukuru sana kwa miaka hii miwili wamepata ushirikiano mzuri kutoka kwa Marine Service Company Limited na kampuni ya ndege ya Fastjet, ambapo mwaka jana walikabidhi vifaa vya kujiokolea (maboya) 500.

Azam marine waleta meli mpya 'Kilimanjaro iv'


                                                                         Kilimanjaro iv
KAMPUNI ya Azam Marine, inaleta boti mpya ya Kilimanjaro iv, ambayo inatarajiwa kuwasili nchini nchini, kuanzia mwishoni wa mwezi huu, ikiwa na uwezo wa kubeba abiria 700 na kutumia muda wa dakika 70 kwa safari moja ya kati ya Zanzibar na Dar es Salaam. Hii ni boti mpya kabisa katika muendelezo wa boti za Kilimanjaro, ambayo itakidhi mahitaji ya wasafiri wa eneo hili kwa kuwa inabeba sifa zote, ambazo ni Usalama, Kasi zaidi na Unadhifu. Kaa tayari kwa mzigo mpya kutoka Azam Marine.

Chanzo: Binzubeiry

HATIMAYE DR. SLAA AKUBALIWA KUOANA NA MPENZI WAKE...

HATIMAYE Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni, imetupilia mbali rufaa iliyokuwa imekatwa na aliyekuwa mume wa Josephine Mushumbusi( KWA  SASA  NI  MCHUMBA WA DR. SLAA) , Maimbo baada ya kuiona rufaa hiyo haina msingi wowote kisheria.

Hukumu hiyo ya rufaa ya  madai ya ndoa Na.32/2012 ilitolewa leo na Hakimu Aniseth Wambura ambapo alisema mahakama yake imefikia uamuzi huo wa kuitupa rufaa hiyo kwasababu haina mantiki ya kisheria.

Hakimu Wambura alisema mahakama yake imekubalina na hukumu iliyotolewa Aprili 2012 na Mahakama ya Mwanzo Sinza katika kesi ya madai talaka iliyokuwa imefunguliwa na Mushumbusi anayetetewa na wakili wa kujitegemea Philemon Mutakyamilwa  dhidi ya Maimbo ambapo mahakama hiyo ya chini ilitangaza kuwa hakukuwa na ndoa baina ya watu hao kwasababu Maimbo alikuwa ni mzinzi, simwaminifu katika ndoa yake na alikuwa akimtesa mkewe.

HALI BADO NI MBAYA MTWARA....WANAFUNZI WAWILI WAMETANDIKWA RISASI, MMOJA AMEFARIKI HAPOHAPO

 Mwandishi wetu aliyepo Mtwara ametueleza kuwa hivi sasa baadhi ya wananchi wa eneo la magomeni mkoani mtwara wamekimbilia katika Hospitali ya Mkoa wa Mtwara Lugula wakihofia usalama wao kutokana na vurugu za kuchomwa kwa nyumba zao pamoja na vibanda vya biashara zilizotokea leo asubuhi katika eneo hilo..
 Maduka maeneo ya Magomeni yamechomwa moto ikiwamo pia mali za Askari magereza . Mwanafunzi wa CHUNO amefikishwa hospitali Ligula na majeraha ya risasi mguuni. 
Mwanamke mwingine anayekadiriwa kuwa na miaka 25 mjamzito ameuawa kwa kupigwa risasi maiti ipo Ligula.

Thursday, May 23, 2013

SHEHA WA TOMONDO- ZANZIBAR ALIYEMWAGIWA TINDIKALI JANA USIKU

Sheha Mohammed Omary Said aliyemwagiwa tindikali na mtu asiyejulikana akiwa katika hospitali ya Mnazi Mmoja Unguja akipatiwa matibabu, Sheikh Mohammed amepata maumivu makali sehemu za kifuwa na jicho kuumia

Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Mjini Magharibi,Mukhadam Khamis,amesema chombo kilichotumika kumwagia tindikali Sheha huyo kilipatikana eneo la tukio na kwamba polisi imekichukua kwa kukichunguza kitaalam ili kugundua aliyekuwa akikitumia kwa kuangalia alama za vidole.

Sheha huyo alimwagiwa tindikali jana usiku wakati alipotoka nje ya nyumba yake kuchota maji na ndipo mhalifu huyo alipomwagia tindikali na kwamba hakuweza kumtambua.

Sheha Mohammed Kidevu akiwa katika wodi ya Hospitali kuu ya Rufaa Mnazi Mmoja akipata matibabu ya majaraha ya kitu kinachosadikiwa kwa Tindi Kali,akipata matibabu hayo katika hospitali hiyo.

RAIS KIKWETE ATANGAZA VITA KUHUSU VURUGU ZA MTWARA.....AMESEMA SERIKALI YAKE ITAWASULUBU WACHOCHEZI WA VURUGU

WAKATI hali ikizidi kuwa tetea Mkaoni Mtwara kufutia Mapigano yaliyoanza jana Mkoani humo Rais Kikwete amevunja ukimwa wake na kutoa amri  wahusika wakuu wa tukio hilo kusakwa mara moja.

Akizungumza katika eneo la Kizota, Dodoma wakati wa kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Barabara ya Dodoma kwenda Iringa, Rais Kikwete  alisema wote waliohusika na vurugu hizo watasakwa na kuchukuliwa hatua kali.

Rais Kikwete alisema rasilimali inayopatikana mahali popote pale nchini inatakiwa kutumiwa na Watanzania wote... “Hivi watu wa  Nyarugusu wadai dhahabu ya pale au kinachopatikana Chalinze basi kisitumiwe na watu wa Morogoro! Hivi tutakuwa na taifa kweli?,”  alihoji kwa ukali Rais Kikwete.

ASKARI ALIYENASWA NA MAGUNIA 18 YA BANGI HUKO HIMO AWATOROKA POLISI

ASKARI Polisi Koplo Edward, anayedaiwa kusafirisha dawa za kulevya (bangi) gunia 18 huko Himo, Kilimanjaro tarehe 18, Mei 2013, ametoroka chini ya ulinzi wa askari polisi saba na kutokomea kusikojulikana.

Mtuhumiwa huyo alikuwa dereva wa gari aina ya Toyota Landcruiser namba PT. 2025 la Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) Mkoa wa Arusha.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas alisema askari huyo akiwa chini ya ulinzi wa askari polisi saba, walikwenda nyumbani kwake kwa ajili ya ukaguzi, na walipofika nyumbani kwa  mtuhumiwa, walimwamini na kumwacha kuingia ndani peke yake nao waliingia ndani ili kuendelea na upekuzi, na ndipo mtuhumiwa alipofungua mlango wa nyuma ya nyumba yake na kukimbia bila ya wao kufanikiwa kumkamata

Alisema polisi imemkamata Inspekta wa Polisi Izaack Manoni aliyekuwa anasimamia upekuzi huo: “Inspekta Manoni yupo chini ya ulinzi na hatua za kinidhamu dhidi yake zitachukuliwa,” alisema ACP Sabas na kuongeza: 

“Mtuhumiwa Edward, anayetafutwa kwa sasa alishafukuzwa kazi, akipatikana atafikishwa mahakama ya kiraia kusomewa mashitaka ya kufanya biashara ya dawa za kulevya,” alisema.

Alisema tayari mtuhumiwa mwenzake ambaye ni askari polisi mwenye namba G. 2434 PC George, amesomewa mashitaka yake jana.

Mbali na mtuhumiwa huyo, watuhumiwa wengine waliokamatwa na magunia 30 ya bangi wilayani Arumeru nao wamepandishwa kizimbani kusomewa mashitaka yao.

via gazeti la MTANZANIA

Magazeti ya leo Alhamisi 23rd May 2013





MKURUGENZI WA MASHITAKA NCHINI ATAKA LWAKATARE ASHITAKIWE KWA UGAIDI TENA

MKURUGENZI wa Mashitaka (DPP), Dk. Eliezer Feleshi, amewasilisha ombi katika Mahakama ya Rufaa nchini, akiomba itengue uamuzi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam wa kumfutia mashitaka matatu ya ugaidi Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Wilfred Lwakatare na Ludovick Joseph.

Dk. Feleshi aliwasilisha ombi hilo juzi kwa njia ya maandishi, ambapo katika maombi yake anaiomba mahakama hiyo iitishe mwenendo wa shauri lililotolewa uamuzi huo na Jaji wa Mahakama Kuu, Lawrence Kaduri Mei 8, mwaka huu na kuupitia upya na ifute uamuzi huo kwa kuwa una makosa kisheria.

Kwa mujibu wa hati ya madai, Dk. Feleshi anadai Mahakama Kuu haikuombwa kumfutia mashitaka Lwakatare kama Jaji Kaduri alivyotoa uamuzi huo, bali aliiomba mahakama iitishe majalada ya kesi ya msingi iliyofunguliwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Machi 18 na 20 mwaka huu.

RASLIMALI ZA NCHI NI MALI YA TAIFA ZIMA....WALIOANDAMANA HUKO MTWARA TUTAWASHITAKI'... RAIS KIKWETE

                                                    Polisi wawasaka waandamanaji Mtwara
Rais wa Tanzania, Jakaya Kikwete amewaonya watu wanaosababisha uvunjifu wa amani nchini humo kuwa watakamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria.

Onyo hilo linafuatia ghasia ambapo ofisi kadha, maduka na nyumba zimechomwa katika mkoa wa Mtwara ulioko kusini mashariki mwa Tanzania jana

Akihutubia kupitia televisheni ya taifa, TBC1, Rais Kikwete amesema wale waliokamatwa na polisi wakati wa ghasia hizo watashitakiwa.

Ghasia hizo zilianza muda mfupi baada ya Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo kuwasilisha bajeti ya wizara yake bungeni. Akizungumzia madai ya waandamanaji hao, Rais Kikwete amesisitiza kuwa raslimali za nchi ni mali ya taifa zima.

BUNGE LAAHIRISHWA TENA LEO MPAKA UFUMBUZI WA GESI MTWARA UTAKAPOJULIKANA


 Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Anna Makinda ameliahirisha tena bunge leo asubuhi ili kupisha kamati ya uongozi ya Bunge iendelee kukutana ili kutoa maamuzi na tamko kuhusu vurugu za Mtwara zilizojotokeza jana na kusababisha mtu mmoja kufariki dunia na uharibifu mbalimbali kutokea ikiwemo kuchomwa moto nyumba za viongozi wa serikali,chama cha mapinduzi na nyumba ya mwandishi wa habari wa TBC.
Pia mjadala wa makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini umesimamishwa kwa muda mpaka ufumbuzi wa tatizo la vurugu hizo utakapopatiwa suluhisho.

Kesho bajeti ya makadirio ya mapato na matumizi ya Afrika Mashariki itajadiliwa.

Wednesday, May 22, 2013

NYUMBA YA MWANDISHI WA HABARI WA TBC YACHOMWA MOTO HUKU MABOMU YAKIRINDIMA HUKO MTWARA

Hali imezidi kuwa mbaya katika Mji wa Mtwara na hivi punde watu wanaendelea kufanya uharibifu katika maeneo mbalimbali ya mji huo.

Jengo moja ambalo linadaiwa kumilikuwa na CCM limechomwa moto katika eneo la Majengo na daraja linalounganisha Lindi na Mtwara limevunjwa.

Mbali na hayo pia nyumba ya mwandishi wa habari wa Shirika la Utangazaji la Tanzania (TBC)imechomwa moto.

Katika Mji wa Mtwara milio ya mabomu na risasi ndio inayosikika kila kona. Jeshi la Polisi linajaribu kuwadhibiti vijana  na watu wengine ambao wanafanya vurugu hizo.