Sunday, November 25, 2012

Tanzania Ready To Send Troops To DRC

Tanzania is ready to send troops to the Democratic Republic of Congo to fight M23 rebels who are making advances to the capital Kinshasa, a minister has said.

Foreign Affairs and International Cooperation minister Bernard Membe said Thursday that the country would, however, only send its troops if the UN headquarters in New York immediately mandated the Southern Africa Development Community (SADC) to deploy troops in DRC.

Presidents from the Great Lakes Region are meeting in Kampala Friday for a crisis summit during which they will discuss the deteriorating situation in eastern DRC where the rebels have captured Goma and Sake, 20km away, and vowed to press on with their offensive to take the South Kivu provincial capital of Bukavu, 300km south of Goma.

Mr Membe said leaders within the region under their chairman, Ugandan President Yoweri Museveni, had called a crisis summit to discuss the matter and see how they could arrest the situation.
The minister said the UN was currently using Chapter 6 of its resolutions, which basically allowed peacekeeping and not peace enforcement. In peace enforcement, the UN troops would, if need be, use force to execute their mandate.

Presently, there were over 17,000 troops under the UN who were not doing much to protect the Congolese people and instead, they were only “observing things”.

“We condemn what the rebels are doing in eastern Congo….it is unacceptable to Tanzania. But there is an International Conference of the Great Lakes Region (ICGLR) in Kampala tomorrow (today), which was called expressly to discuss the matter,” Mr Membe said.

He said the situation in eastern Congo had huge impact on all East African states and, if left unchecked, would result in huge numbers of refugees and internally displaced people.

Source: http://www.africareview.com

Chadema Uongozi Balaa

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeitafutia dawa migogoro inayotokana na baadhi ya makada wake kuonyesha nia ya kuwania urais na ubunge mwaka 2015, baada ya kuanzisha utaratibu maalumu wa wanachama wake kugombea nafasi mbalimbali za uongozi.

Kwa mujibu wa taarifa zilizolifikia gageti  hili, mpango huo unakuja wakati Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Zitto Kabwe ametangaza nia ya kugombea urais katika uchaguzi mkuu ujao, kitendo ambacho kiliwashtua vigogo wa chama hicho akiwamo mwasisi wake, Edwin Mtei.

Mara kadhaa Mtei amekuwa akimwonya Zitto kuwa kitendo chake cha kutangaza nia yake ya kugombea urais kitasababisha mzozo na mpasuko ndani ya chama hicho.

Mtei amekuwa akisema kuwa Zitto anatakiwa kuwaunganisha wanaChadema na siyo kuwagawa, au kuwavuruga na kwamba siyo shida kuonyesha hisia za kuwania urais, lakini tatizo ni kuwa hali hiyo inatengeneza mzozo mkubwa.


Mtei ambaye aliwahi kuwa Waziri wa Fedha na Gavana wa Benki Kuu (BOT) enzi za utawala wa Mwalimu Julius Nyerere, alisema wakati mwafaka ukiwadia, Chadema kitaamua ni nani mwenye sifa za kugombea urais akisema kina utaratibu wake wa kuwapata wagombea mbalimbali wa uongozi.

Akizungumza wakati akijibu hoja mbalimbali katika mtandao wa Jamii Forum katikati ya wiki hii, Zitto ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini, alisema viongozi wa chama hicho walikutana mjini Morogoro hivi karibuni na kutengeneza utaratibu wa watu kutangaza nia wanapotaka kugombea nafasi yoyote ya uongozi.

“Nadhani huu ni uamuzi mzuri wa chama maana watu wengine wana wasiwasi usio na msingi wowote kwamba kuwa na wagombea wengi kwenye chama ni kuvuruga chama,” alisema Zitto na kuongeza:

“Lakini watu haohao wanashangilia kweli wakiona demokrasia inavyotekelezwa kwenye nchi nyingine kama Marekani. Alisema kuwa tatizo la Watanzania wanapenda kuona demokrasia inatekelezwa, lakini wao wanaogopa kuitekeleza, hivyo mwongozo kwa wagombea ambao walipitisha Morogoro utasaidia sana.“Uamuzi wa Morogoro kuhusu mwongozo kwa wagombea utatusaidia sana kuondoa mashaka kama haya,” alisema Zitto.

Mwananchi Jumapili lilipomuuliza Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa chama hicho, John Mnyika kuhusu jambo hilo  alionyesha kutofahamu lolote kuhusu utaratibu huo, wala ulipofanyika huo mkutano wa Morogoro.

“Mkutano upi wa Morogoro?” alihoji Mnyika. Alipoelezwa kuwa suala hilo lilizungumzwa na Zitto katika Mtandao wa Jamii Forum alisema: “Muulize kwanza Zitto akupe ufafanuzi ni kikao gani cha chama, pia juu ya huo utaratibu, akikueleza ndiyo urudi tena kwangu.”

Juhudi za kumpata Zitto kueleza kwa undani kuhusu utaratibu huo hazikuzaa matunda, kwani simu yake ya mkononi ilikuwa ikiita bila majibu, baadaye kuzimwa kabisa. Akizungumzia azma yake ya kuachana na ubunge kama alivyoahidi mwaka 2005 kuwa, atagombea vipindi viwili pekee Zitto, alisema kuwa aliwaambia wapigakura wake kwamba nia yake ni kuwa rais wa nchi.

“Nia yangu ni kupisha wengine nao wakimbize kijiti cha maendeleo ya jimbo letu na mkoa wetu,” alisema Zitto na kufafanua, “ Nimeshasema mara kwa mara kwamba ukiachana na siasa kazi ninayoipenda zaidi ni ualimu.”

Alisema kuwa akiachana na ubunge atakwenda kufundisha kwa kuwa anapenda kufanya tafiti, kusoma, kuandika na kufundisha.

“Hivi sasa tunaandaa mpango wa kuanzisha Chuo Kikuu cha Ziwa Tanganyika (Lake Tanganyika) mkoani Kigoma, nitafurahi kama nitakuwa mmoja wa wahadhiri wa mwanzo wa chuo hiki,” alisema Zitto.

Katika uchaguzi Mkuu wa mwaka 2005, Mwenyekiti wa Chama hicho, Freeman Mbowe alisimama kugombea nafasi ya urais akishindana na Rais Jakaya Kikwete ambaye alikuwa akisimama kwa mara ya kwanza.

Mwaka 2010, Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Willbrod Slaa aligombea nafasi hiyo na kuibuka mshindi wa pili kwa kupata asilimia 26.34 nyuma ya Rais Kikwete ambaye alipata asilimia 61.17.

Hivi sasa tayari kumetokea maneno ya chinichini miongoni mwa wabunge waliopo madarakani wakiwatuhumu baadhi ya wanachama wa chama hicho ambao wameaanza kuingia katika majimbo yao kutaka kugombea viti hivyo katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

Wabunge hao wanahoji kama wanachama hao wanaofanya hivyo wanataka kugombea ubunge katika uchaguzi ujao ili kukifanya chama kiongeze idadi ya wabunge bungeni, kwa nini wasiende kugombea katika majimbo ambayo hayana  wabunge wa chama hicho?Vilevile, chama hicho kilipata msukosuko katika mchakato wa kupata wabunge wa Viti Maalumu katika uchaguzi uliopita na kulazimika kuweka vigezo ambavyo viliondoa manung’uniko hayo.

Baadhi ya vigezo hivyo ni elimu, mchango wa mgombea katika chama, wanawake waliogombea katika majimbo na uzoefu katika ubunge.

Chanzo:  http://www.mwananchi.co.tz/habari

Umewahi kuusikia Wimbo wa Bahati Bukuku Unaumiza Soma hapa chini


MWIMBAJI mahiri wa Injili Bongo, Bahati John Bukuku (pichani chini) yuko kwenye mchakato wa kutinga kortini kwa ajili ya kumburuza mumewe, Daniel Basila ili atoe talaka.

Kwa mujibu wa chanzo, Bahati ambaye wimbo wake wa Dunia Haina Huruma ameuchezea filamu, ataenda mahakamani Jumatatu ya keshokutwa lengo likiwa kuitaka sheria imsaidie aweze kupata hati ya talaka ya kutengana na mwanaume huyo ambaye haishi naye kwa miaka sita sasa.

“Bahati anasema lengo la Daniel ni kumuweka njia panda ndiyo maana aliahidi kwenda mahakamani wiki mbili zilizopita ili ashughulikie talaka lakini hakufanya hivyo, sasa Jumatatu atakwenda mwenyewe,” kilisema chanzo.

Wakati huohuo, habari zinadai kwamba Daniel amekuwa akisema wimbo wa mkewe, Dunia Haina Huruma ametungiwa yeye kama kijembe.

Risasi Jumamosi liliwasaka wote wawili kwa nyakati tofauti ili kujua ukweli wa madai hayo.

Bahati: “Mimi ninachotaka ni talaka, aliahidi mbele ya kaka yangu kwamba angeshughulikia wiki mbili zilizopita, lakini hajafanya hivyo. Kwa hiyo mimi kwenda mbele ya sheria ni sawa tu. Huo wimbo namshangaaa, kama aliwahi kufumaniwa basi kweli ni wake.”

Basila: “Nilibanwa na mambo, lakini nakumbuka ahadi, nitaitekeleza lakini naomba isiwe kwa presha sana. Kuhusu wimbo lini nimesema alinitungia mimi?”

Kutoka Global Publisher

Magazeti ya leo Jumapili 25th November 2012


MATOKEO YOTE YA PREMIER LEAGUE NOV 24 NA WAFUNGAJI WAKE YAKO HAPA.



                              

Kinana Awataka Mawaziri Kufanya Kazi Kwa Kasi...!

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM), Abdulrahaman Kinana, amewataka mawaziri wa Serikali ya awamu ya nne kufanya kazi kwa kasi ili kutekeleza ilani ya uchaguzi kwani wakishindwa kufanya hivyo watawajibishwa na chama.Alisema chama hakitawavumilia mawaziri ambao hawatekelezi majukumu yao na kukifanya chama hicho kichukiwe na wananchi.

Alisema kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (Nec) mawaziri watakuwa wakitoa taarifa za utendaji kazi na kwamba wajumbe wa Nec watawabana kwa maswali ili kupata ufafanuzi wa kina katika masuala mbalimbali ya wizara zao.Alisema kila waziri, mbunge na Diwani anayetokana na chama hicho atakuwa akipimwa utendaji wake katika kuwahudumia wananchi wa eneo lake na taifa kwa ujumla.
Kinana alisema hakuna kiongozi yeyote wa Serikali aliyejuu ya chama hicho bali chama kipo juu yao na ni wajibu wao kuwa watiifu kwa chama na wananchi wakati wote wa utekelezaji wa majukumu yao.

“Naomba ieleweke kwamba CCM imejipanga katika kuwaunganisha na kuwahudumia Watanzania, hivi sasa tunaanza utaratibu mpya ambapo mawaziri watakuwa wakitoa maelezo.
Alisema kama kuna kiongozi ambaye ataona kuwa kasi yetu ni kubwa ni bora akaachia ngazi.

Akizungumzia makundi ndani ya chama hicho , Kinana alisema kuwa tangu ulipomalizika uchaguzi wa ndani kuna baadhi ya viongozi walioshindwa wamekuwa wabinafsi kwa kutochaguliwa katika nafasi za uongozi hali inayowafanya kujiona bora kuliko wengine.

Alisema kutokana na hali hiyo kuna baadhi ya makada wa CCM wamekuwa wabinafsi huku wakiibuka na sababu mbalimbali ikiwamo rushwa.
“Watu wamekuwa wabinafsi kwa kukosa nafasi za kuchaguliwa ndani ya chama. Kama hakupita anaibuka na sababu lukuki na hata kudai aliyechaguliwa hafai bali yeye ndiye anayefaa,” alisema.

Kinana akizungumzia utendaji kazi wa mawaziri alisema kuanzia kikao kijacho cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, watakuwa wakitoa taarifa hizo ambapo wajumbe wa NEC watawabana kwa maswali na kuhitaji ufafanuzi wa kina katika masuala mbalimbali ya wizara zao.

Alisema kila Waziri, Mbunge na Diwani anayetokana na chama hicho atakuwa akipimwa utendaji wake katika kuwahudumia wananchi wa eneo lake na Taifa kwa ujumla.
Alisema hakuna kiongozi yoyote wa Serikali aliyekuwa juu ya chama bali chama kipo juu yao na wajibu wao kuwa watiifu kwa chama na wananchi wakati wote wa utekelezaji wa majukumu yao.

“Ninapenda ifahamike sasa CCM, imejipanga katika kuwaunganisha na kuwahudumia Watanzania, hivi sasa tunaanza utaratibu mpya ambapo Mawaziri watakuwa wakitoa taarifa zao katika vikao vya NEC na kuhojiwa maswali na wajumbe.

“Kila Waziri atahojiwa utendaji wa shughuli za Serikali katika Wizara yake na utekelezaji wa ilani na ikiwa kuna atakayeonekana kuwa hafai hatua zitachukuliwa stahiki zitachukuliwa.