Wednesday, May 1, 2013

"NITAGOMBEA URAIS MWAKA 2015 ENDAPO WANANCHI WENGI WATANIOMBA NIFANYE HIVYO"....BENARD MEMBE

WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe, amesema atakuwa tayari kuwania urais mwaka 2015, iwapo wananchi wataona anafaa na kumtaka afanye hivyo.

Alisema hayo juzi wakati akijibu maswali ya mwandishi wa habari hii mjini Iringa, baada ya kumalizika kwa kongamano la vyuo vya elimu ya juu mkoani hapa, lililofanyika katika ukumbi wa St. Dominic.

Membe aliyekuwa mgeni rasmi katika kongamano hilo, alisema ingawa muda wa kufanya uamuzi kuhusu mwaka 2015 bado na chama hakijatoa utaratibu, lakini atasubiri ushauri wa Watanzania.

"Naomba kurudia, mimi nilishapata kuueleza umma kuwa muda bado haujafika wa kutangaza kugombea urais ...ila nasema hivi natarajia sana ushauri wa Watanzania.

JK akutana na Morgan Tsvangirai ikulu, Dar

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiteta jambo na Waziri Mkuu wa nchi ya Zimbabwe Bwana Morgan Tsvangirai ikulu jijini Dar es Salaam. Chanzo: Freddy Maro

Bilionea wa Man city kuanzisha timu mpya MLS

                             Sheikh Mansour (katikati) anataka kuwekeza MLS dola Milioni 100

MMILIKI wa Manchester City, Sheikh Mansour wa Abu Dhabi yupo karibuni kuwekeza kiasi cha dola za Kimarekani, Milioni 100 kuanzisha timu mpya itakayoshiriki katika Ligi Kuu ya Marekani, ijulikanayo kama Major League Soccer ambayo itakuwa na maskani New York.

Bilionea huyo wa waliokuwa mabingwa wa Ligi Kuu England, amekuwa katika mazungumzo mazito na ya siri na MLS kwa miezi kadhaa juu ya kuingiza timu mpya ya nguvu USA.

Sheikh ana matumaini yeye na Maofisa wa MLS, watakuwa kwenye nafasi ya kutangaza mpango huo wakati kikosi cha Roberto Mancini kitakapokwenda Marekani kucheza na Chelsea Jijini New York katika mchezo maalum wa hisani mwishoni mwa mwezi ujao.

DEREVA WA “BODA BODA” AKAMATWA NA SHORTGUN, RISASI SITA

GEDSC DIGITAL CAMERAPichani juu ni bunduki aina ya Shortgun Mossberg ikiwa na risasi sita ambayo ilikutwa kwenye begi la dereva huyo wa Boda boda aliyekamatwa na polisi tarehe 28.04.2013 (Picha na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha)

Jeshi la Polisi Mkoani hapa limemkamata mtu mmoja aitwaye Ally Rashid Salimu (23) Mwendesha pikipiki za abiria maarufu kwa jina la “Boda Boda” mkazi wa kata ya Sombetini jijini hapa akiwa na bunduki aina ya shortgun Mossberg yenye namba T292166 ikiwa na risasi sita.Akizungumza na

waandishi wa habari ofisini kwake leo saa 5:30 asubuhi Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Liberatus Sabas alisema kwamba, tukio hilo lilitokea juzi tarehe 28.04.2013 muda wa saa 3:00 asubuhi katika maeneo ya Shamsi yaliyopo jijini hapa.

Magazeti ya leo jumatano ya 1st May 2013





HALI ILIVYO LEO ASUBUHI JIJINI ARUSHA TUKISHEREKEA SIKU YA MEI MOSI

BAADA YA MIEZI 9 YA BILA KUONEKANA HADHARANI, HII NDIO PICHA MPYA ALIYOPIGWA MZEE MANDELA HIVI KARIBUNI

Baada ya kipindi kirefu cha Rais wa zamani wa Afrika Kusini Nelson Mandela kutoonekana hadharani hatimae picha yake ya kwanza baada ya miezi tisa imeonekana.

Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini aliongozana na watu wengine kwenda kumtembelea Mzee Mandela ambapo baada ya kumuona, Zuma amesema afya ya Mzee iko vizuri sasa hivi japokua amekonda kidogo.