Monday, September 24, 2012

KAMATI KUU YA CCM YAKUTANA DODOMA, WAWANIA UONGOZI 'PRESHA' JUU

 Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akiwasili ukumbini kuendesha kikao cha Kamati Kuu ya CCM mjini Dodoma leo. Kushoto ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohammed Sheni na Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Pius Msekwa na Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama.
 Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akiendesha kikao cha Kamati Kuu ya CCM, mjini Dodoma leo. Kushoto ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohammed Sheni na Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Pius Msekwa na Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama
  Katika Mkuu wa CCM, Wilson Mukama akisoma utangulizi, mwanzoni wa kikao cha Kamati Kuu ya CCM mjini Dodoma leo. Kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya  Kikwete na kulia ni Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Pius  Msekwa
 Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Waziri Mkuu Mizengo Pinda, akiwaslimia wajumbe wa Kamati Kuu, Mjumbe wa NEC, Uchumi na Fedha Mwigulu Nchemba, Mjumbe wa NEC Oganaizeshenu, Asha Abdallah Juma na Naibu Katibu Mkuu wa CCM, (Zanzibar Vuai Ali Vuai) kabla ya kuanza kukao cha Kamati Kuu ya CCM mjini Dodoma leo
  Wajumbe wa Kamati Kuu, Maua Daftari na Simba wakijadili jambo taratibu, kabla ya Kikao cha kamati hiyo kuanza leo mjini Dodoma
 Baadhi ya viongozi wa CCM wanaowania nafasi mbalimbali za uongozi kwa awamu nyingine katika uchaguzi mkuu wa CCM utakaofanyika Novemba mwaka huu, wakiwa nje ya ukumbi wakati kikao cha Kamati Kuu kikiendelea mjini Dodoma. Kutoka kushoto ni, Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Kigoma, Azim Premji, Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Rukwa, Hypolitus-Rukwa, Wajumbe wa NEC Asha Baraka na Hkadija Kopa
Anthony Dialo (kulia) akijadili jambo na wenzake nje ya ukumbi

Hakika Maharusi Wamependeza sana Kiasili jamani tudumisha mila za Kiafrika

                                                   Mrs & Mrs Ibrahimu hakika mmependeza







NIMEIPENDE HII MUNGU WETU HASHINDWI KITU HASA UKIMTUMAINIA

MASTAA wa filamu Bongo ambao ni wanandoa, Juma Kilowoko ‘Sajuki’ na Wastara Juma hivi karibuni waliwaacha watu hoi kufuatia vituko walivyokuwa wakivionesha, Ijumaa Wikienda liliwanasa kwenye shughuli.

Wawili hao walionesha vituko hivyo kwenye harusi ya mdogo wa Wastara aitwaye Latifa Juma iliyofanyika mwishoni mwa wiki, Tabata jijini Dar.

Katika sherehe hiyo, Wastara aliamua kuweka matatizo yao pembeni na kuanza kukata nyonga kwa staili iliyowaacha hoi maharusi pamoja na watu wengine waliokuwepo kwenye ‘mnuso’ huo.

Achilia mbali hilo, Sajuki naye alipoingia ukumbini hapo aliingia kwa staili ya kucheza kiduku huku mkononi akiwa ameshika kimfuko cha bisi ‘pop corn’.

Vituko havikuishia hapo kwani kuna wakati Wastara alipotakiwa kufika mbele kukata keki, Sajuki alimfuata kwa nyuma na kumshikia gauni lake refu kama mpambe wake na keki ilipokatwa alichukua kipande na kukila hata kabla ya maharusi.

Mpaka wawili hao wanaondoka ukumbini hapo, walikuwa wameacha gumzo kutokana na matukio yao ambayo yaliifanya sherehe hiyo ifane.

Magazeti ya leo Jumatatu 24th September 2012