Friday, February 8, 2013

MSIKUBALI KUDANGANYWA ANGALIENI MAFANIKIO YENU- PALANGYO

WANACHAMA wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Meru,mkoani Arusha,wameshauriwa kutokukubali kudanganywa na Vyama vya kisiasa ambavyo vinaeneza Propaganda chafu  kuwa hakuna kilichofanyika tangia Uhuru,badala yake wachukie siasa zinazosababisha uvunjifu wa amani

KAMPUNI YA NDEGE YA fastjet YAKANUSHA UVUMI KUWA IMEFUTIWA LESENI YA BIASHARA

Jean Uku Meneja Masoko na Mauzo wa Kampuni ya ndege ya Fastjet akizungumza na waandishi wa habari kwenye hoteli ya Hyyat Regency Dar es salaam kukanusha uvumi wa habari zinazosema kampuni hiyo imenyang’anywa leseni ya kufanya biashari nchini Tanzania, Kushoto ni Givaldine Dawe Meneja Utawala.

Pamoja na habari zilizoandikwa na kusemwa kwenye vyombo vya habari leo, biashara ndani ya kampuni ya fastjet inaendelea kama kawaida. Madai yanayotukabili ya kunyang’anywa leseni hayana ukweli wowote. Tunaendelea kufanya kazi na ndege zetu nchini Tanzania kama kawaida na bado tunazidi kuzindua vituo vipya kama ilivyopangwa. Huu ni uzushi wa baadhi ya watu au kampuni zenye chuki dhidi ya kampuni ya fastjet, kusudi lao ni kudhoofisha uaminifu na kuharibu sifa ya jina la biashara na bidhaa zetu za fastjet.

Ofisi zetu na vituo vyetu vya kuuzia tiketi bado viko wazi kwa ajili ya bookings na Kwa tiketi zilizolipiwa pesa haitarudishwa.

TAMKO RASMI BAADA YA MASAA MACHACHE

MAGUNIA MENGINE 97 YA BANGI YAKAMATWA NA JESHI LA POLISI ARUSHA

 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi wa Polisi Liberatus Sabas akiwaonyesha waandishi wa habari madawa ya kulevya aina ya bangi ambayo yalikuwa kwenye magunia 97 yaliyokamatwa na askari wa jeshi hilo katika eneo la Usa river wilayani Arumeru (Picha na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi)

HIVI NDIVYO MATUMAINI ALIVYOPOKELEWA JIJINI DAR

    Matumaini (katikati) akisaidiwa na wasanii wenzake muda mfupi baada ya kutua.
   Matumaini (kulia) akiwa na Bi. Mwenda (wa pili kushoto) na anayefuata (kushoto) ni msanii mwenzake Kiwewe wakisubiri gari la kumpeleka hospitali.
                                     Bi. Mwenda akiwa amembeba Matumaini mgongoni.

Yaliyojiri Magazetini Leo Ijumaa ya 8th February 2013