Friday, September 21, 2012

REDD’S MISS TEMEKE KUZOA MIL 1.5 LEO (Sept 21)

                                     Mariedo kuwavika magauni, viatu vya kisasa

MALKIA atakayetwaa taji la Redd’s Miss Temeke 2012 katika shindano linalofanyika Ijumaa Sept 21 katika ukumbi wa PTA(SabaSaba Hall), atajinyakulia zawadi zinazofikia milioni 1.5 sanjari na tiketi ya moja kwa moja kushiriki shindano la Redd’s Miss Tanzania baadaye mwaka huu.

Katika mlolongo huo wa zawadi, mshindi wa kwanza atajinyakulia fedha taslim Sh. Milioni 1. Mshindi wa pili atajinyakulia fedha taslim Sh.laki nane wakati mshindi wa tatu atapata Sh. Laki saba na washindi wote watatu kila mmoja atajipatia nguo ya kutokea jioni sanjari na viatu, vikiwa na thamani ya kila mmoja Sh. Laki  5.

Duka la kisasa la Mariedo Boutique itatoa gauni la Sh.350,000 na kiatu cha Sh 150,000 kila mmoja kwa washindi hao watatu wa kwanza watakaoshinda. Mbali ya washindi hao, mshindi wa nne atajinyakulia kitita cha Sh. 400,000 ambapomshindi wa tano ataondoka na Sh 300,000 wakati warembo wengine wote watakaosalia kila mmoja atapata Sh.200.000.

Ikiwa ni funga dimba ya mashindano ya urembo ya kanda nchini, shindano hilo litanogeshwa na wasanii wanaong’ara katika luninga, Mpoki wa kundi la Komed Original na Steve Nyerere ambaye mbali ya kuigiza sauti za watu mbalimbali, pia ametoa filamu kadhaa kwa siku za hivi karibuni.

Mbali ya wasanii hao, bendi ya Mashujaa Musica,yenye wanamuziki nguli kama Charles Baba, MCD, Ferguson, Ali Akida sanjari na wanennguaji kama Lilian Internet na wengineo pia itanogesha usiku huo.

Taji la Redd’s Miss Temeke, linashikiliwa na mrembo Husna Twalib. Warembo wa Miss Temeke wamekuwa wakijifua kwa wiki tatu sasa chini ya ukufunzi wa Leyla Bhanji, ambaye amekuwa akisaidiwa pia na warembo wa miaka ya nyuma wa Miss Temeke akiwemo, Regina Mosha(20020, Hawa Ismail(2003), washiriki wa mwaka jana Joyce Maweda, Mwajabu Juma, Cynthia Kimasha na katika shoo wamekuwa na Dickson Daud kutoka kundi la THT.

Shoo ya ufunguzi itakuwa tofauti kabisa na shoo nyingine yeyote iliyowahi kuyanyika nchini, kwani imezingatia zaidi urembo na nini msichana anatakiwa kufanya na si unenguaji tu. Warembo 15 wanatoka katika vitongoji vya Kigamboni, Kurasini na Chang’ombe ambapo kila sehemu wametoka warembo watano ambapo washindi watatu wa kwanza watapata fursa ya moja kwa moja kushiriki Redds Miss Tanzania 2012.

Warembo hao ni Agness Goodluck, Angela Gasper, Flaviana Maeda,Edna Sylvester, Catherine Masumbigana, Khadija Kombo, Neema Doreen, Flora Kazungu, Lilian Joseph, Elizabeth Peter, Elizabeth Boniphace, Jesca Haule, Zulfa Bundala, Mariam Ntakisivya na Esther Albert.

Mbali ya Redd’s, Miss Temeke 2012 pia imedhaminiwa na City Sports Lounge, Jambo Leo, Mariedo Boutique, Global Publishers, Dodoma Wine, Push Mobile, Mariedo Boutique, 100.5 Times FM, Kitwe General Traders, Fredito Entertainment, katejoshy.blogsport.com na 88.4 Cloud’s FM.

Temeke imewahi kutwaa taji la Miss Tanzania mara tatu, kupitia warembo Happiness Sosthenes Magesse aka Millen mwaka 2001, Sylvia Remmy Baham mwaka 2003 na Genevieve Mpangala. Lakini pia imetoa warembo waliowahi kushika nafasi ya pili na tano bora katika Miss Tanzania kama Jokate Mwegelo, Irene Uwoya, Irene Kiwia, Queen David, Cecylia Assey, Sabrina Slim, Miriam Odemba, Ediltruda Kalikawe na Asela Magaka.

Matatizo yetu tuyachukulie kama changamoto kimaisha!

NDUGU zangu, matatizo katika maisha ni kitu cha kawaida sana. Hakuna anayeweza kuyaepuka kwani yapo kwa ajili ya binadamu na ndiyo maana hakuna anayeweza kupitisha siku bila kukumbwa na tatizo aidha dogo ama kubwa. Lakini, utafiti unaonesha kuwa miongoni mwetu wapo watu wanapokumbwa na matatizo hushindwa kuyachukulia kuwa ni kitu cha kawaida, badala yake wanaishia kwenye kuvunjika mioyo na kukata tamaa kabisa ya maisha.

Ni wazi binadamu tunatofautiana katika namna tunavyoyapokea matatizo pale yanapotukabili, lakini baadhi ya watu wanapitiliza katika namna wanavyoyapokea kwani inafikia wakati mtu anapopatwa na tatizo huingia katika hali fulani ya kuona dunia ni mbaya na maisha ni yenye upendeleo.

Anashindwa kuyaangalia matatizo hayo kwa umakini na kuyakubali kisha kuangalia namna ya kuyatatua, hali ambayo huweza kusababisha tatizo kuzidi kuwa kubwa na kumuathiri zaidi.

Katika maisha tunapoingia katika hali kama hiyo ni sawa na kujizuia kusonga mbele katika kupata ama kutafuta kile ambacho tunakitaka katika maisha yetu ya kila siku.

Hii ni kutokana na ukweli kwamba, hali ya kukata tamaa inapopiga hodi katika nafsi zetu huwa tunashindwa kufanya yale ambayo ni ya muhimu kwetu na kuishia kwenye kusononeka.

Wengine wanapopatwa na matatizo badala ya kuyatafutia ufumbuzi, hupandwa na hasira na wakati mwingine kuchukua maamuzi ambayo hayastahili.

Kwa mfano umekuwa katika uhusiano na mtu ambaye ulitokea kumpenda sana lakini ikafikia kipindi ukamkosa aidha baada ya kufariki ama kuachana. Au fikiria umepata barua ya kuachishwa kazi au kama ni mwanafunzi umefeli katika masomo yako yote, hivi utajisikiaje?

Wapo ambao wamefikia hatua ya kukatisha maisha yao kwa kukumbwa na matatizo kama hayo. Lakini je, huo ndiyo ufumbuzi sahihi? Hatuoni kwamba kwa kufanya hivyo ni sawa na kukufuru? Ukweli ni kwamba, matatizo hayachagui mtu, humtokea kila mtu na wakati wowote lakini pia yana ufumbuzi wake. Hivyo basi unapokumbwa na matatizo si vizuri kuanza kunung’unika bali fanya kila uwezalo kutafuta ufumbuzi tena kwa kutumia mbinu sahihi.

Ninachopenda kushauri ni kwamba, kama unasumbuliwa na tatizo fulani si wakati wa kukata tamaa na kuona kwamba huna haki ya kuendelea kuishi.

Fahamu unayo nafasi ya kukabiliana vilivyo na matatizo hayo. Elewa unapokabiliwa na tatizo fulani kisha ukashindwa kutafuta ufumbuzi, unaweza kulifanya tatizo likawa kubwa zaidi ama kuzua tatizo lingine.

Epukana sana na mrundikano wa matatizo ambayo hayakutafutiwa ufumbuzi kwani kwa kufanya hivyo unahatarisha maisha yako lakini pia chukulia kwamba kila tatizo linalokupata ni changamoto tu za kimaisha.

Magazeti ya leo Ijumaa 21st September 2012


Tupo Mjini Arusha Stand kubwa ya Mabasi Jengo la Namvua Plaza gorofa ya pili Tonga Tailoring