Monday, September 10, 2012

Maazimio Ya Kamati Kuu Ya Chadema

1.Uwajibikaji wa kisiasa wa viongozi wa serikali na idara zake.,Waziri Emmanuel Nchimbi,IGP Mwema,Paul Chagonja,RPC Morogoro na Kamanda wa FFU,na RPC IRINGA na Kamanda wa FFU wajiuzulu na au wafukuzwe kazi

2.RPC Morogoro na Iringa,makamanda wa FFU Morogoro na Iringa,na maaskari waliouwa wakamatwe mara moja na kufunguliwa mashitaka

3.Rais aunde tume huru ya uchunguzi wa vifo tata katika matukio ya kisiasa.1.ARUSHA vifo 3.IGUNGA,vifo vingi havijulikani bado,3.ARUMERU MASHARIKI,vifo 5, 4.SINGIDA kifo 1, MOROGORO na IRINGA
chadema haitatambua wala kushirikiana na kamati batili ya NCHIMBI.

4.Msajili wa vyama vya siasa John Tendwa ni mtu hatari kwa taifa kwa kauli tata anazozitoa.anashirikiana na au anajipendekeza kwa CCM na Serikali yake.CHADEMA tangu sasa haitafanya kazi na Tendwa wala kufanya mawasiliano naye ya kiofisi.Labda kama atagundua makosa yake na kuomba msamaha,chadema itatafakari namna ya kufanya naye kazi tena.

5.TBC TAIFA Television na Redio ni hatari kwa taifa,kwa kubobea kupotosha umma juu ya matukio mengi.Hivyo CHADEMA Inatangaza mgogoro na TBC na inaelekeza na kuomba wanachama ,wapenzi,na wananchi wote wapendao ukweli na haki,kuisusia TBC

6.Jeshi la Polisi lijue kuwa Maandamano ndiyo siasa yenyewe na mikutano ya hadhara ni lazima kwa mawasiliano ya umma na siasa.kuzuia vitu hivyo ni kunyima wananchi haki yao ya kikatiba ya uhuru wa kukusanyika na kutoa maoni,pia kupata habari na taarifa

7.Operesheni MOVEMENT FOR CHANGE M4C,Inaendelea kadiri ya ratiba ilivyopangwa katika utaratibu uleule uliokuwepo awali.Inarejea Iringa Siku si nyingi.Na kamati kuu Imetoa msisitizo MAALUM kwa jimbo mojawapo singida,ambapo wamesema watatumia helcopita,magari,pikipiki na baiskeli na miguu,na badala ya kupita vijijini kama majimbo mengine,Chadema wanasema kwa sababu maalum katika jimbo hilo watapita kitongojikwa kitongoji,ili kufunza adabu baadhi ya viongozi (msisitizo ni wa msoma MAAZIMIO.jimbo hili laweza kuwa la Mwigullu Mchemba,kadiri ya wanahabari waliokuwepo)

8.Kutokana na mgogoro wa muda mrefu mkoani mwanza uliosababisha meye wa chadema kuvuliwa umeya kinyume na utaratibu na kwa njama za CCM na Serikali,na bahati mbaya sana kwa kushirikisha madiwani wa CHADEMA,KAMATI KUU imewavua UANACHAMA madiwani wake wawli 1 ADAMU CHAGULANI wa kata ya IGOMA na HENRY MATATA wa KITANGIRI, PIA uongozi wote wa CHADEMA mkoa wa mwanza Umevunjwa.

Imesomwa na Mwenyekiti CHADEMA Taifa

JK Katika Mkutano Wa Kampala

Mhe. Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipitia waraka wenye makubaliano kabla ya yeye  na Wakuu wenzake wa  Nchi na Serikali  za Ukanda wa Maziwa Makuu kuuweka sahihi baada ya mkutano wao uliofanyika Septemba 8, 2012 katika Hoteli ya Speke Resort Munyonyo mjini Kampala, Uganda.

PICHA NA IKULU

RATIBA YA MECHI ZA CHAN 2014 NDIO HII, TAIFA STARS INAHUSIKA PIA.

                                                   Soccer city Johannesburg South Africa.

Timu ya taifa Taifa stars imepangiwa kucheza na Uganda (The Cranes) kwenye raundi ya kwanza ya michuano ya kuwania ticket ya kucheza fainali za Afrika kwa wachezaji wa ndani (ChAN) zitakazofanyika Afrika Kusini 2014.

Ratiba iliyopangwa sept 7 2012 kwenye makao makuu ya shirikisho la mpira wa miguu Afrika (CAF) mjini Cairo inaonyesha Tanzania imeingia moja kwa moja raundi ya kwanza ambapo itacheza na Uganda.

Mechi ya kwanza itachezwa uwanja wa taifa Dar es salaam kati ya june 21,22 na 23 2013 wakati marudiano itakua uwanja wa Mandela Namboole jijini Kampala kati ya july 5,6 na 7 2013.

Nchi 38 zinashiriki kwenye hizo mechi za mchujo ambapo nyingine zitaanzia raundi ya awali itakayochezwa kati ya november 30 na december 1 na 2 mwaka huu wakati mechi za marudiano zitakua kati ya December 14, 15 na 16.

Ratiba imepangwa kwa makundi ya kanda ambapo jumla ya timu 16 ndizo zitakazocheza fainali hizo nchini Afrika kusini, kanda ya kaskazini itapeleka timu mbili katika fainali, kanda ya magharibi A pia timu mbili, Magharibi B timu tatu, Kanda ya kati timu tatu, Kanda ya kati mashariki timu tatu, kanda ya kusini timu tatu akiwemo mwenyeji Afrika Kusini.

Kwa upande wa kanda ya Tanzania (Kati mashariki) timu zinazoanzia raundi ya awali ni Burundi, Eritrea, Ethiopia na Kenya ambapo kama hufahamu fainali za kwanza za CHAN zilifanyika Ivory Coast 2009 ambapo Tanzania ilishiriki lakini mshindi alikua Congo DRC na fainali za pili zilifanyika 2011 nchini Sudan ambapo Tunisia ndio ilichukua ubingwa.

Fainali za kwanza zilishirikisha timu nane kabla ya kuongezwa hadi 16 za sasa.

Magazeti ya leo Jumatatu 10th September 2012