Saturday, November 17, 2012

Nchi Tatu Zakabidhiwa Tuzo

Nchi tatu zimekabidhiwa Tunzo kutokana na ubunifu wao katika Sekta ya Umma .

Nchi hizo zilizoshinda na kupewa Tunzo na Jumuiya ya Utumishi wa Umma katika Afrika na Uongozi AAPAM ni pamoja na Kenya, Mauritius na Ghana

Tunzo hizo zimetokana na kuwa wabunifu katika masuala mbalimbali ambapo Kenya imekuwa mshindi wa Kwanza kwa kupata medali ya dhahabu ikifuatiwa na Mauritius iliyopata Medali ya Fedha na Ghana iliyopata Medali ya Shaba.

Wakati huo huo Mkutano wa 34 wa AAPAM uliomalizika hivi leo hapa Zanzibar na kufungwa rasmi na Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Balozi Seif Ali Idd umetoa maazimio mbalimbali yanayohusu Mkutano huo.

Miongoni mwa maazimio hayo ni kuwa na Mfumo bora na mzuri wa Utawala, kuimarisha mazingira juu ya nchi na Uongozi, Kuwashirikisha wadau wengine katika kuimarisha Utawala Bora na siyo Serikali kujipangia wao wenyewe tu.

Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa AAPAM ameeleza kuwa Mkutano huo wa 34 umefanikiwa sana kutokana na mahudhurio ambapo Wajumbe 420 walihudhuria kutoka nchi 35 za Afrika na nje ya Afrika.

Mwaka jana Mkutano kama huo wa AAPAM uliofanyika nchini Malawi nchi 35 zilihudhuria ambapo wajumbe wapatao 210 ndio walioshiriki.

Katibu huyo wa AAPAM ameeleza kuwa tangu kufanyika Mikutano hiyo hii ni mara ya kwanza kwa wajumbe wengi kuhudhuria katika Mkutano huo na kuwa wa mafanikio makubwa.

Mkutano wa AAPAM hapo mwakani umeamuliwa kufanyika mjini Kigali,Rwanda.

Wajumbe kadhaa waliohudhuria Mkutano huo wameshaanza kuondoka hapa Zanzibar kurejea nyumbani.

IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR.

Safu ya Mkapa yarejea CCM

KUNA kila dalili kuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete amekirejesha chama hicho katika mikono ya Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa, baada ya kuwateua katika nafasi za juu za CCM waliokuwa wasaidizi wa mtangulizi wake huyo.

Wasaidizi hao ni pamoja na Makamu Wenyeviti, Philip Mangula (Tanzania Bara) na Dk Ali Mohamed Shein (Tanzania Zanzibar) pamoja na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahaman Kinana, ambao walichaguliwa na kuteuliwa katika vikao vya juu vya CCM vilivyomalizika hivi karibuni mjini Dodoma.

Baadhi ya wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanasema kwamba lengo la mabadiliko yaliyofanywa ni kujaribu kurejesha utaratibu wa CCM kuisimamia Serikali, utamaduni ambao ni kama ulikuwa umekufa, tangu Serikali ya awamu ya nne ilipoingia madarakani.

Mhadhiri wa zamani wa Chuo cha Ushirika Moshi, Akwiline Kinabo anasema kwamba kuna kila dalili kuwa Mkapa ana ushawishi katika uteuzi wa safu mpya katika sekretarieti ya chama hicho.

“Inawezekana Mangula, Kinana na Dk Shein walifanya vizuri sana enzi za Mkapa hadi akashawishi waingizwe kwenye sekretarieti ya sasa, lakini enzi za Mkapa na sasa ni kama mlima na kichuguu,” alisema.


Endelea nayo...www.kwanzajamii.com/?p=4356

Magazeti ya leo Jumamosi ya 18th November 2012