Tuesday, March 5, 2013

JOHN MNYIKA APANGA KUITISHA MAANDAMANO MAKUBWA MACHI 26

Mbunge wa Jimbo la Ubungo JOHN MNYIKA amesema Ofisi yake imepanga kuitisha Maandamano makubwa Machi 16 Mwaka huu kuelekea Ofisi za Wizara ya Maji, kutokana na Wizara hiyo kushindwa kulipatia ufumbuzi suala la upatikanaji wa Majisafi pamoja na uondoaji wa Majitaka katika maeneo mbalimbali ya Jimbo hilo.

Akizungumza na CLOUDS FM, MNYIKA amesema kuwa tayari Ofisi yake imekamilisha hatua za msingi za uratibu wa maandano hayo, ikiwa ni pamoja na kulishirikisha Jeshi la Polisi pamoja na Uongozi wa Manispaa ya Kinondoni.

Amebainisha kuwa licha ya ofisi yake kulifikisha suala la tatizo la Maji katika baadhi ya maeneo ya Jimbo hilo Wizarani sambamba na kuwasilisha hoja Binafsi bungeni, hakuna hatua zozote za awali zilizochukuliwa huku Wakazi wa maeneo hayo wakitaabika kwa kukosa maji.

"HAZIPITI SIKU MBILI BILA KULIZWA NA KERO ZA WAANDISHI WA HABARI:.....MAMA KANUMBA

Mama yake mzazi na marehemu Steven Kanumba amesema maswali anayoulizwa kila mara na waandishi wa habari hasa za udaku humfanya asipitishe siku mbili bila kulia kutokana na kumkumbuka mwanae kipenzi.

Akiongea na kipindi cha The Avenue cha TBC 1, mama huyo ambaye hivi karibuni amejiingiza kwenye uigizaji wa filamu pia amesema mara nyingi anapofuatwa na waandishi wa habari kumuuliza maswali kuhusiana na mwanae hubaki akilia na waandishi wa habari huishia kuandika habari za uongo tofauti na alivyoongea.

“Kupoteza mtoto wa miaka 28 sio mchezo, inauma,” alisema Mama Kanumba.

Aliongeza kuwa hawezi kuangalia filamu za mwanae kwakuwa humfanya ajisikie vibaya japo nguo zake bado zipo na huziona kila siku.