Thursday, November 29, 2012

VIONGOZI WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI WAZINDUA BARABARA YA ARUSHA-NAMANGA-ATHI RIVER

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi Kenya Jumatano Novemba 28, 2012 tayari kuhudhuria sherehe za ufunguzi wa barabara ya Arusha-Namanga-Athi River pamoja na Mkutano wa Wakuu wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki utaozungumzia maendeleo ya miundombinu. Kiongozi wa Jumuiya ya Waislamu wa Ismailia Mtukufu Aga Khan naye alikuwepo hapo uwanjani.
                            Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipanda mti wakati wa uzinduzi wa barabara hiyo
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete na viongozi wenzie wa nchi wanachama za Jumuiya ya Afrika Mashariki wakikata utepe kwa pamoja kuzindua  rasmi wa Barabara ya Arusha – Namanga – Athi River yenye  urefu wa kilometa 104.4 kwa upande wa Tanzania




 Baadhi ya mawaziri na makatibu wakuu wa Tanzania waliohudhuria sherehe za uzinduzi rasmi wa barabara ya Arusha – Namanga – Athi River yenye  urefu wa kilometa 104.4 kwa upande wa Tanzania
              Rais Jakaya Kikwete akitoaa hotuba yake wakati wa uzinduzi wa barabara hiyo





Rais Jakaya Mrisho Kikwete na viongozi wenzie wa nchi wanachama za Jumuiya ya Afrika Mashariki wakifurahia mara baada ya kuzindua rasmi ujenzi wa barabara hiyo kwa kukata utepe.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na viongozi wenzie wa nchi wanachama za Jumuiya ya Afrika Mashariki  wakiwa katika picha ya pamoja na wadau mbalimbali waliofanikisha ujenzi wa barabara ya Arusha – Namanga      

Makamu Wa Rais Dkt. Bilal Aagana Na Rais Wa Kenya Mwai Kibaki

  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na Rais wa Kenya, Mwai Kibaki, ambaye ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro, mara baada ya ufunguzi wa Jengo la ofisi za Jumuiya hiyo iliyofanyika Jijini Arusha jana, Nove 28, 2012.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipunga mkono kuwaaga wananchi baada ya kumsindikiza Rais wa Kenya, Mwai Kibaki, ambaye ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro, mara baada ya ufunguzi wa Jengo la ofisi za Jumuiya hiyo iliyofanyika Jijini Arusha jana, Nove 28, 2012

Maadhimisho Kupinga Ukatili Dhidi Ya Wanawake

                                                                  Mkuu wa mkoa wa singida
 Kikundi cha nyota njema kikitumbuiza ngoma ya asili ya kabila la Kinyaturu wakati wa maadhimisho ya siku ya kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia

SERIKALI imeyataka mashirika ya kiraia kushirikiana pamoja, ili kupiga vita na hatimaye kutokomeza kabisa vitendo vinavyosababisha ukatili wa kijinsia, hususani wanavyofanyiwa wanawake na watoto wadogo nchini.

Hayo yamebainishwa mjini Singida na mkuu wa mkoa huo, Dk. Parseko Kone, kwenye maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili dhidi ya wanawake, yaliyoadhimishwa kitaifa katika viwanja vya Peoples, mjini Singida, jana.

Maadhimisho hayo, yamefanyika mkoani Singida, kwa ushirikiano wa mashirika 16 hapa nchini, yaliyoipa dhamana ya kusimamia sherehe hizo, shirika la Action Aid-Singida,huku kauli mbiu yake ikiwa ‘FUNGUKA! Kemea ukatili dhidi ya wanawake, sote tuwajibike’.

Dk. Kone alisema kuwa, kutokana na changamoto nyingi zinazowakabili wanawake ikiwemo ukatili wanaofanyiwa na wanaume, serikali kwa kushirikiana na mashirika ya kirai bado yanayo kazi kubwa katika kuungana pamoja ili kutokomeza unyanyasaji huo.

“Madhara yatokanayo na ukatili kwa wanwake katika jamii hupunguza nguvu kazi ya Taifa, baadhi ya madhara ya ukatili huo ni mauaji ya wanawake, ulemavu wa kudumu wa viungo…kupungua kwa uzalishaji kwa kuwa mwanamke ndiye mzalishaji mkuu kwenye kaya nyingi hapa nchini,”alisema Dk. Kone.

Mapema akimkaribisha mgeni rasmi katika maadhimisho hayo, mkuu wa wilaya Singida mwalimu Queen Mlozi aliagiza kuwa ni vema sherehe kubwa kama hiyo inapofanyika mkoani hapa, wahusika wakashirikisha serikali ili iweze kufana zaidi.

Mwalimu Mlozi alilazimika kutoa amri hiyo, baada ya maadalizi, husani hamasa kuwa katika kiwango cha chini sana, hali iliyochangia uwanja kuonekana mtupu kutokana na watu wachache sana kujitokeza, vikiwemo vikundi vichache vya hamasa.

“Jamani ni vizuri maadhimisho makubwa kama haya yanapoletwa mkoani kwetu, basi wahusika wajitahidi kushirikisha serikali washirikiane pamoja kuhamasisha wananchi ili wajitokeze kwa wingi na wafurike kwenye sherehe,”alisema kwa masikitiko Mlozi.

Akizungumzia maadhimisho hayo, Juliana Bwire, afisa usawa na jinsi wa shirika la Concern worldwide kutoka jijini Dar es Salaam alisema siku 16 walizokuwa Singida, walizitumia vijijini kuielimisha jamii madhara ya ukatili, ikiwemo unyanyasaji, ukeketaji, na wanawake kunyimwa haki.

Aidha mmoja wa wanawake waliohudhuria sherehe hizo, Happynes Juma(30) mzaliwa wa Kigoma, alieleza kwa masikitiko ukatili aliofanyiwa na mumewe ikiwemo kudaiwa hajui kufanya mapenzi, hali iliyoleta mgogoro wa kifamilia na suala hilo lipo ustawi wa jamii, tayari kwa ajili ya kutengana.

Alisema maadhimsho hayo yatahitimishwa jijini Dar es Salaam siku ya desemba 8, mwaka huu.

Na Elisante John;Singida
Novemba 28,2012.

Hotuba Ya JK Bunge La Afrika Mashariki

Honourable Speaker;
Invited Speakers here present;
 Honourable Members of the East African Legislative Assembly, Distinguished Guests; Ladies and Gentlemen;

 I thank you, Hon. Speaker for giving me this rare opportunity to address this august Assembly at its 3rd sitting since its inauguration this year. I also thank you for the kind words you have spoken about me and my dear country, the United Republic of Tanzania.

Honourable Speaker; Since I am speaking to Members of East African Legislative Assembly for the first time since you were elected, let me take this opportunity to extend to you all my warm congratulations on your well deserved election. Your election is a testimony of the immense confidence and trust reposed in you. More so I wish to .... Read More... http://www.kwanzajamii.com

Jengo La Jumuiya Ya Afika Mashariki Lazinduliwa

  Rais Jakaya Mrisho Kikwete na viongozi wenzie wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakiangalia mfano wa jengo jipya la makao makuu ya Jumuiya hiyo pamoja na maelezo yake baada ya kulifungua rasmi  Novemba 28, 2012 jijini Arusha
                     Mfano wa  jengo la Makao makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete na viongozi wenzie wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakifunua pazia  kufungua rasmi jengo jipya la makao makuu ya Jumuiya  Novemba 28, 2012 jijini Arusha
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na wakuu wenzie wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakiwa katika picha ya pamoja na wadau pamoja na wabunge wa Afrika Mashariki

PICHA NA IKULU

Mkuu Wa Wilaya Na Nape Wamzika Sharobaro

  Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye (Watatu kulia, waliobeba jeneza) akishiriki kubeba jeneza lenye mwili wa aliyekuwa msanii wa muziki wa kizazi kipya na filamu, Hussein Ramadhani maarufu kwa jina la Sharo Milionea, alipokiwakilisha Chama Cha Mapinduzi, kwenye mazishi ya msanii huyo, leo kwenye Kijiji cha  Lusanga, Muheza Tanga.
 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akitoa pole za Chama Cha Mapinduzi (CCM) alipokiwakilisha Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwenye mazishi ya aliyekuwa msanii wa muziki wa kizazi kipya na filamu, Hussein Ramadhani maarufu kwa jina la Sharo Milionea,leo kwenye Kijiji cha  Lusanga, Muheza Tanga
 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nauye, akitupa mchanga kaburini, alipokiwakilisha Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwenye mazishi ya aliyekuwa msanii wa muziki wa kizazi kipya na filamu, Hussein Ramadhani maarufu kwa jina la Sharo Milionea,leo kwenye Kijiji cha  Lusanga, Muheza Tanga.
 Mkuu wa wilaya ya Muheza, Subra Mgalu akisoma salam za Shirika la Fursa Sawa kwa Wote (EOTF) la Mama  Anna Mkapa, kwenye msiba huo. Pamoja naye ni Nape

 (Picha na Bashir Nkoromo).

Safari Ya Mwisho Ya Sharo Milionea

MAELFU ya waombolezaji jana walijitokeza kushiriki mazishi ya msanii Hussein Ramadhan maarufu kwa jina la Sharo Milionea, huku mamia wakizirai baada ya kushindwa kujizuia wakati mwili wake unawekwa kaburini.

Mwili wa msanii huyo ulizikwa jana kijijini kwake Lusanga wilayani Muheza saa 7 mchana, katika tukio lililomshirikisha Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye ambaye alimwakilisha mwenyekiti wa chama hicho, Rais Jakaya Kikwete.

Waombolezaji walianza kumiminika kijijini Lusanga tangu juzi jioni na idadi yao iliongezeka zaidi jana asubuhi. Mkuu wa Wilaya ya Muheza, Subira Mgalu ndiye aliyekuwa mwenyekiti wa Kamati ya Mazishi.Sala ya mazishi iliongozwa na Sheikh Twaha Juma ambaye baadaye aliamuru jeneza hilo kupelekwa makaburini, ambako waombolezaji kadhaa walipoteza fahamu.20 wapelekwa hospitali

Miongoni mwa matukio yaliyojitokeza katika msiba huo ni baadhi ya waombolezaji kupoteza fahamu msibani.Matukio tofauti ya watu kuzirai yalitokea wakati mwili wa msanii huyo ulipokuwa unapelekwa nyumbani kwao kijijini Lusanga ukitokea Hospitali Teule ya Wilaya ambako ulihifadhiwa tangu alipopata ajali Jumatatu usiku na wakati wa mazishi.

Miongoni mwa waliopoteza fahamu katika msiba huo ni wasanii na waigizaji wa filamu waliokuwa wakiigiza na Sharo Milionea wakati akiwa katika kundi la AL Riyam.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na MC wa shughuli hiyo, Steve Nyerere, zaidi ya watu 20 walipoteza fahamu katika msiba huo na kupelekwa katika Hospitali ya Wilaya ya Muheza.

mbolezaji kutokuwa na shaka juu ya waliopoteza fahamu kwa kuwa madaktari maalumu walikuwa wameandaliwa hospitalini hapo kwa ajili ya kuwapa huduma.

Mwananchi lilifika katika hospitali Teule na kukuta waliokuwa wamepoteza fahamu, wengi wao wakiwa ni wasichana, wakipata huduma huku wengine wakiomba kupewa ruhusa ili wakahudhurie maziko.

JK atuma rambirambi
Rais Jakaya Kikwete amemtumia salamu za rambirambi, Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Dk Fenella Mukangara kutokana na vifo vya wasanii watatu vilivyotokea hivi karibuni, kikiwamo cha Sharo Milionea.

Taarifa iliyotolewa jana Dar es Salaam na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, ilisema kuwa Rais Kikwete ameshtushwa na vifo hivyo vya ghafla.

Wasanii hao ambao walifariki dunia katika mazingira tofauti ni Mwigizaji wa Kundi la Kaole, Khalid Mohamed ‘Mlopelo’ aliyefariki dunia hivi karibuni kutokana na maradhi yaliyokuwa yanamsumbua kwa muda mrefu.

Soma zaidi:  http://www.mwananchi.co.tz/habari