Tuesday, July 10, 2012

KOCHA MKUU WA TAIFA STARS KUWA MGENI RASMI LIGI YA KUIBUA VIPAJI

  KOCHA mkuu wa timu ya Tanzania(Taifa Stars),Kim Poulsen anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye mashindano ya ligi ya ya kuibua vipaji vya soka la vijana inayojulikana kama Moivaro Youth Football League(MYFL) ambayo itatimua vumbi mnamo septemba 29 mwaka huu mkoani Arusha.

Pia,viongozi mbalimbali wa ngazi za soka mkoani Arusha na nchini kwa ujumla akiwemo mtaalamu wa masuala ya ufundi wa shirikisho la soka nchini(TFF),Sunday Kayuni anatarajiwa kuwa miongoni mwa wageni walioalikwa katika ligi hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mkurugenzi na mwasisi wa Taasisi ya Future Stars Aademy ya jijini hapa,Alfred Itaeli alisema kwamba ligi hiyo itashirikisha timu za wanawake pia ambapo usajili wa timzu zitakazoshiriki  unataraji kuanza Agosti 18 mwaka huu.

Itaeli ,alisema kwamba kabla ya  ligi hiyo kutimua vumbi wameandaa mafunzo ya wiki mbili kwa waamuzi  wenye umri  kati ya miaka 8 hadi 15 ambao watatumika kuchezesha ligi hiyo ili kuepuka gharama za kukodi waamuzi mbalimbali ambapo mafunzo hayo yatandeshwa na mwamuzi mkongwe nchini Billy Mwilima.

Alitaja lengo kuu la ligi hiyo ni kukuza vipaji vya soka nchini na kuweka ushindani kwa kila rika huku akisisitiza kuwa kwa kuwa ligi hiyo haina wadhamini wameamua kutoza kiasi cha sh,100,000 kama ada za kiingilio.

Na Ashura Mohamed-Arusha

No comments: