Thursday, August 2, 2012

BAADA YA MWAKA, PROFESA MWANDOSYA AINGIA BUNGENI KWA MARA YA KWANZA, ALIYOYASEMA NDIO HAYA!

Profesa Mark Mwandosya akiwa na Waziri mkuu Mizengo Pinda alipokwenda kumtembelea wakati akiumwa, hii ilikua May 7 2012.

Jumatano Aug 1 2012 nilikua nimetulia nachek bunge ghafla nikaona wabunge wanapiga meza kama kuna shangwe flani hivi, kuja kushtuka kumbe ilikua ni kutokana na waziri wa ofisi ya Rais aisekua na wizara maalum Profesa Mark Mwandosya kuingia bungeni kwa mara ya kwanza baada ya kuugua kwa zaidi ya mwaka mmoja.

Alisema “naona mkono wake mwenyezi Mungu katika uponyaji wangu, ni zaidi ya mwaka tangu nimekwenda kwa ajili ya matibabu na sijazungumza katika bunge hili tukufu, moja kati ya mambo nilikua nasema mbona ungenirudishia hata kwa dakika tano nije kuongea na wabunge wenzangu na mwenyezi Mungu ameliridhia ombi langu”

Pamoja na kuwashukuru na kuwasifu viongozi wote waliomjulia hali wa chama tawala na upinzani, Profesa Mwandosya amesema “afya ni muhimu sana na tuendelee kupima afya zetu wabunge, mimi miaka 45 sijawahi kuona kitanda hospitali nimekwenda kukikuta huko Hydrebad, nilidhani ni mtu mwenye afya sana mtu wa mazoezi kila siku asubuhi na jioni lakini kumbe mwili wa binadamu Mungu alivyoumba ni maajabu yake yeye mwenyewe”

Thanks kwa : http://millardayo.com/

No comments: