Monday, August 6, 2012

HUYU NDIO MCHEZAJI ALIESAJILIWA NA SIMBA NA LEO.

Klabu ya Simba imeendelea kufungua milango yake katika soko la usajili baada ya wiki iliyopita kumtwaa Mbuyi Twite na Mrisho Ngassa, leo hii klabu hiyo imemsajili kiungo wake wa zamani aliyekuwa akiichezea Azam Fc Ramadhan Chombo Redondo.

Taarifa rasmi kutoka kwa Redondo mwenyewe ni kweli amesaini mkataba na Simba akitokea Azam baada ya mkataba wake kumalizika, ambapo  Shaffihdauda.com imemkariri akisema “Nimesaini mkataba wa miaka miwili na Simba nikiwa mchezaji huru baada ya mkataba wangu na mwajiri wangu wa zamani  Azam kumalizika”

Redondo ambaye aliondoka Simba miaka 3 iliyopita, amesaini Simba kwa ada ya millioni 3 ambapo leo wakati akisaini amepewa shilingi millioni 20 na millioni 10 baadae.

No comments: