Saturday, November 17, 2012

Safu ya Mkapa yarejea CCM

KUNA kila dalili kuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete amekirejesha chama hicho katika mikono ya Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa, baada ya kuwateua katika nafasi za juu za CCM waliokuwa wasaidizi wa mtangulizi wake huyo.

Wasaidizi hao ni pamoja na Makamu Wenyeviti, Philip Mangula (Tanzania Bara) na Dk Ali Mohamed Shein (Tanzania Zanzibar) pamoja na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahaman Kinana, ambao walichaguliwa na kuteuliwa katika vikao vya juu vya CCM vilivyomalizika hivi karibuni mjini Dodoma.

Baadhi ya wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanasema kwamba lengo la mabadiliko yaliyofanywa ni kujaribu kurejesha utaratibu wa CCM kuisimamia Serikali, utamaduni ambao ni kama ulikuwa umekufa, tangu Serikali ya awamu ya nne ilipoingia madarakani.

Mhadhiri wa zamani wa Chuo cha Ushirika Moshi, Akwiline Kinabo anasema kwamba kuna kila dalili kuwa Mkapa ana ushawishi katika uteuzi wa safu mpya katika sekretarieti ya chama hicho.

“Inawezekana Mangula, Kinana na Dk Shein walifanya vizuri sana enzi za Mkapa hadi akashawishi waingizwe kwenye sekretarieti ya sasa, lakini enzi za Mkapa na sasa ni kama mlima na kichuguu,” alisema.


Endelea nayo...www.kwanzajamii.com/?p=4356

No comments: