Saturday, June 29, 2013

NDEGE YA OBAMA NI NYUMBA INAYOTEMBEA AIR Force One ni ndege kubwa ya Rais wa Marekani. Ndege hii ina sifa nyingi kama ndege nyingine, lakini ina nyongeza ambayo kwenye ndege nyingine hakuna. Air Force One ambayo imewahi kuchezewa filamu iliyoitwa kwa jina hilohilo na staa wa muvi za Hollywood, Harrison Ford imeonekana ndiyo ndege yenye usalama zaidi duniani. SIFA KUBWA: Ndani ya ndege hiyo kuna ofisi ya rais, jiko, chumba cha mikutano, bafu, sehemu ya kuvalia nguo, eneo la kufanyia mazoezi ‘gym’ na chumba cha mawasiliano. Ndiyo maana inasemwa ni nyumba inayotembea. Pia kuna chumba cha maafisa wanaomlinda rais, sehemu yao ya kufanyia mkutano wakipata dharura na zahanati kama rais akiugua ghafla wakati ndege ipo angani. Si hayo tu, kuna chumba chenye simu 85 za mezani na Tivii 19 kwa ajili ya kupata habari za kidunia wakati ndege ipo juu. Ndege hiyo haikamiliki kuiita Air Force One bila kutambulisha sehemu maalum ambayo hutumika kijeshi kumkwepesha adui anayetaka kuilenga kwa lengo la kuilipua.

 AIR Force One ni ndege kubwa ya Rais wa Marekani. Ndege hii ina sifa nyingi kama ndege nyingine, lakini ina nyongeza  ambayo kwenye ndege nyingine hakuna.

Air Force One ambayo imewahi kuchezewa filamu iliyoitwa kwa jina hilohilo na staa wa muvi za Hollywood, Harrison Ford imeonekana ndiyo ndege yenye usalama zaidi duniani.
SIFA KUBWA:
Ndani ya ndege hiyo kuna ofisi ya rais, jiko, chumba cha mikutano, bafu, sehemu ya kuvalia nguo, eneo la kufanyia mazoezi ‘gym’ na chumba cha mawasiliano. Ndiyo maana inasemwa ni nyumba inayotembea.

Pia kuna chumba cha maafisa wanaomlinda rais, sehemu yao ya kufanyia mkutano wakipata dharura na zahanati kama rais akiugua ghafla wakati ndege ipo angani.

Si hayo tu, kuna chumba chenye simu 85 za mezani na Tivii 19 kwa ajili ya kupata habari za kidunia wakati ndege ipo juu.

Ndege hiyo haikamiliki kuiita Air Force One bila kutambulisha sehemu maalum ambayo hutumika kijeshi kumkwepesha adui anayetaka kuilenga kwa lengo la kuilipua.



No comments: