Monday, March 11, 2013

Mashabiki wapendekeza albam mpya ya Lady Jaydee iitwe ‘Nothing But the Truth’

Lady Jaydee leo aliwaomba mashabiki wake wamchagulie jina la albam yake mpya ambapo aliwataka wachague kati ya The Queen is Back na Nothing But the Truth. Mashabiki wake wengi wamependekeza jina la albam yake liwe Nothing But the Truth.

Wiki hii Lady Jaydee ameachia wimbo wake mpya aliomshirikisha Profesa Jay, Joto, Hasira. Pia March 3, msanii huyo mkongwe nchini alimalizia kushoot video ya wimbo huo huku muongozaji akiwa ni Adam Juma.Tayari Joto, Hasira unapatikana kwenye mtandao wa itunes.

No comments: