Tuesday, July 24, 2012

.UKIMWI USIOSIKIA DAWA AFRIKA MASHARIKI NDIO HUU.

                                                        Makao Makuu ya WHO Geneva.
Inawezekana stori nyingine huwa unazichukulia poa, lakini hii usiichukulie poa hata kidogo.

Ninachotaka kukwambia ni kwamba aina ya ugonjwa wa ukimwi ambao hausikii dawa umekua ukiongozeka kwenye hili bara la Afrika katika muda wa muongo mmoja uliopita.

BBC wamesema, kuna ripoti ilimeandikwa na wataalam kwenye jarida la kisayansi la Lancet, ambapo uchunguzi kwa watu 26,000 ndio umekuja na hayo majibu.

Wataalamu hao wamesema hali hiyo ya ugonjwa kutosikia dawa huenda ikatokea ikiwa wagonjwa hawata zingatia na kutumia dawa walizopewa na pia ufuatiliaji mbaya.

hali hiyo inazusha hofu zaidi katika bara la Afrika ambako hakuna njia mbadala ya kuwatibu wanaouguwa maradhi ya Ukimwi.

Watatifi kutoka shirika la Afya duniani-WHO na chuo kikuu London wamegundua kwamba aina ya ukimiwi ambao hausikii dawa unapatikana zaidi kwenye nchi za Afrika Mashariki, Rwanda, Burundi, Kenya, Tanzania na Uganda.

Yani wanasema asilimia 26% ya waathirika wako katika hali hiyo ikilinganishwa na asilimia 14 katika nchi zilizo kusini mwa Afrika
Lakini kwenye nchi za mwa Marekani, Afrika Magharibi na kati hakuna kitu kama hicho.

Chanzo kikubwa cha hayo yote ni kwa sababu wagonjwa hawatumii dawa ipaswavyo.

Hii stori imetoka siku tano tu baada ya kumsikia waziri mkuu Mizengo Pinda akiamplfy habari njema kuhusu maambukizi ya vizuri vya ukimwi kupungua Tanzania.

No comments: