Friday, August 17, 2012

BELINA AWA BALOZI WA NYWELE

                                                 Mwanamitindo Belina Mgeni.

MWANAMITINDO mwenye mvuto Bongo, Belina Mgeni amelamba shavu la nguvu kutoka kwa kampuni kubwa ya nywele nchini kwa kusainishwa mkataba wa mwaka mmoja kuwa balozi wa kampuni hiyo.

‘Akisemezana’ na Motomoto Newz, Belina alisema anamshukuru  Mungu kwa kupata shavu hilo ambapo sasa picha zake zitakuwa zikionekana katika mabango ya kampuni hiyo, pia atakuwa akisuka bure nywele kwa kipindi cha mwaka mmoja na kutumia bidhaa za kampuni hiyo kama balozi.

Aidha, mwanamitindo huyo alisema ataubeba ubalozi huo kwa umakini mkubwa  kwa sababu heshima waliyompa ni kubwa sana  kwa upande wa warembo  na wanamitindo wa hapa nchini.

Na Imelda Mtema

No comments: