Sunday, August 5, 2012

JANUARI MAKAMBA AONGOZA MKUTANO WA WANABUMBULI JIJINI DAR ES SALAAM JANA

 Mbunge wa jimbo la Bumbuli Mhe. January Makamba akiongea na wakazi kutoka wilaya ya  Lushoto jimbo la Bumbuli katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam leo mkutano huo ulikuwa  unajadili maendeleo ya jimbo la  Bumbuli na kutambulisha shirika la maendeleo la  Bumbuli, January Makamba amesema katika kipindi cha mwaka 2011-2012 kiwango cha elimu ya wilaya hiyo imekuwa chini na kusababisha vijana wengi katika mkoa wa Tanga kuwa na sifa ya kuuza chipsi na kubeba mizigo badala ya kufanya kazi kwenye makampuni.
   Wakazi kutoka jimbo la bumbuli wakiwa katika mkutano huo wa kujadili maendeleo ya wilaya ya Bumbuli
          Kikundi cha ngoma kijulikanacho Mount  Usambara Voice kikitoa burudani katika mkutano huo
 Mkurugenzi wa shirika la Bumbuli Bw. Najim Msenga (kushoto), mwenyekiti mteule wilaya ya Bumbuli Bw. Amiri Sheiza (kulia)katibu wa CCM wilaya ya Lushoto Bw. Loth Ole Lemeirut (katikati)wakijadiliana jambo mara baada ya kumalizika kwa mkutano huo
Katibu wa CCM wilaya ya Lushoto Bw. Loth Ole Lemeirut (kushoto)na mwanakamati wa shirika la Bumbuli Bw. Naaman Shauri wakifuatilia kwa umakini mada iliokuwa ikendelea katika mkutato huo Jana

No comments: