Monday, August 27, 2012

Morogoro: Viongozi wa CHADEMA wakamatwa na polisi, vurugu zaibuka!

                 Askari waliokuwa katika eneo la tukio kabla ya kuanza kwa maandamano hayo

                     Gari la chadema lililokuwa likiongoza maandamano hayo
                Mmoja wa kiongozi wa chadema akiwa amekamatwa akiwa ndani ya gari la polisi
Wafuasi wa chadema wakiwa na maandamao hayo mjini morogoro

                      Mwanachama wa Chadema Aliyepingwa Risasi Na kupotesa Maisha
            Moshi wa mabomu yaliolipuliwa kutawanya maandamano ya chadema leo mjini morogoro

Habari kutoka Morogoro zimetufikia hivi punde kutoka chanzo cha uhakika nguvu ya umma imeshinda watu wanaendelea na maandamano baada ya Mabomu kushindwa kutawanya watu. Hali ni tete polisi wamelegea mabomu yamewaishia watu wanasonga mbele

Ni kweli. Polisi wamevuruga maandamano yaliyokuwa yafanyike kwenda eneo la mkutano, Uwanja wa Ndege, hapa Morogoro Mjini. Wamedhalilisha viongozi waliowakamata na sasa wameanza kuomba samahani, yaishe.

Kamanda wa Polisi Morogoro, Shilogile (mnaojua alihamishwa Dar es Salaam kuja hapa...) amevunja makubaliano yaliyofanyika mara mbili ya kuruhusu maandamano. Tunajua wapo wanasiasa hapa Morogoro ambao hawataki meseji ifike leo kwa wakazi wa Morogoro Mjini.

Inajulikana namna ambavyo CCM wamekuwa shaken big time na operesheni iliyokuwa na mafanikio huko vijijini, itawaumiza zaidi ikifanikiwa hapa mjini. Kwa hiyo lengo hapa si kuvuruga tu maandamano, bali ni kuvuruga mkutano, ili hatimaye watu waogope kuja mkutanoni, ujumbe usifike. Hawatafanikiwa kwa hilo, maana wananchi sasa wanazidi kujikusanya, maeneo kama ya Masika, kwenda eneo la mikutano, kwa maandamano.

Polisi wanachafua mji sasa, polisi wanawapitisha wana-Morogoro kwenye tanuru ambalo watu wa Mwanza, Mbeya, Arusha, Moshi, Musoma, Tarime, Ruaha na kwingineko kwingi, walipita/kupitishwa ili kuwa hapo walipo wakiwa na imani isiyoyumba katika mapambano haya ya kudai na kuwaandaa Watanzania kwa mabadiliko makubwa ya kimfumo na kiutawala. Chuma hakiwezi kuwa chuma mpaka kipite kwenye tanuru, lakini why doing it unnecessary?

Tutawapatia more updates on the issue?

No comments: