Saturday, September 29, 2012

ERMIE ATAMBULISHWA KUWA KOCHA WA YANGA

                                                Kocha Mpya wa Yanga katika utambulisho

Hatimaye leo hii klabu bingwa ya Afrika mashariki na kati Dar Young Africans imemtambulisha rasmi kocha wake mpya Mholanzi Ernie Brandts.

Kocha huyu ambaye miezi michache iliyopita alikuwa mwalimu wa klabu bingwa ya Rwanda, APR aliwasili jijini Dar es Salaam jana usiku na leo asubuhi ametambulishwa rasmi kwa waandishi wa habari na kusaini mkataba wa mwaka mmoja wa kuifundisha klabu hiyo ya Jangwani.

Brandts ambaye amewahi kuwa mchezaji wa timu ya taifa ya Uholanzi na klabu kubwa ya nchi hiyo PSV Eindhoven akicheza kwenye nafasi ya ulinzi, amekuja Yanga kuchukua nafasi ya mbelgiji Tom Saintfiest aliyetimuliwa wiki iliyopita baada ya kukaa kwenye klabu hiyo kwa siku 81.

SOURCE: Shaffihdauda.com

No comments: