Tuesday, November 6, 2012

JINSI MASHABIKI WA SIMBA WALIVYOANDAMANA, NA MAJINA YA WANAOTAKA WAONDOKE SIMBA.

Mashabiki wa Simba novemba 5 2012 waliandamana mpaka makao makuu ya club hiyo Msimbazi Kariakoo Dar es salaam wakiwa na mabango mbalimbali yanayomaanisha wamechoka na ishu mbalimbali za club hiyo.

Mabango mengine yalisomeka kwamba mamluki wajirekebishe Simba mmeikuta, mengine Ndugu Kaburu kocha wetu Milovan mchango wake mkubwa bado tunamuhitaji, Kaseja tuachie timu yetu.

Hiyo yote imetokana na Simba kufungwa 2-0 na Mtibwa Sugar novemba 4 2012 Morogoro.

Baada ya kichapo hicho katika msimamo wa ligi kwa timu kongwe jijini Dar es Salaam, YANGA SC imepanda kileleni mwa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baada ya kuifunga Azam FC 2-0 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Ushindi huo unaifanya Yanga iongoze Ligi Kuu kwa kufikisha pointi 26 ikiwa imebakiza mechi moja ya mzunguko wa kwanza dhidi ya Caostal Union mjini Tanga ikifuatiwa na Simba SC yenye pointi 23 ambayo  imefungwa 2-0 na Mtibwa Sugar Morogoro.

Nawakariri baadhi ya mashabiki walioandamana wakisema “tumefungwa kwa sababu ya Kaseja, kamuingilia kocha kapanga timu tumefungwa, huyu mtoto mpaka anapata dhambi… alikua hadaki mechi ya jana, kwanza tunajua kiwango chake kimeshuka na inasemekana na yeye anahusika kwenye kababu, kama anachukua hela imani yake yeye mwenyewe ila sisi tunachojua uwezo hana wa kuidakia timu yetu ya Simba, sio swala la kufungwa tu isipokua ni mwenendo mzima wa Simba Sc kuwa na matatizo ambayo yako sehemu mbili, kwa wachezaji ambao wana matabaka na viongozi pia wana matabaka, viongozi wameshindwa kuiongoza timu”

No comments: