Saturday, November 10, 2012

Wanajeshi Wa Marekani Waadhibiwa

Wanajeshi saba wamarekani wa kitengo cha Elite akiwemo mmoja wa maafisa wa jeshi aliyehusika na kumkamata na kumuua Osama bin Laden wameadhibiwa kwa madai ya kutoa taarifa za siri za marekani kinyume na sheria.

Kuvunjwa kwa usalama huo kunadaiwa kujiri wakati wanajeshi hao walikuwa wakifanya kazi ya kutoa huduma za ushauri katika kutengeneza mchezo wa video inayoonyesha makabiliano ya kijeshi.

Saba hao walipata barua za nidhamu na kupokea nusu ya mishahara yao kwa kipindi cha miezi miwili .

Idara ya usalama ya marekani bado inachunguza iwapo maafisa zaidi wa kitengo cha Seal walihusika

Chanzo:  http://www.bbc.co.uk/swahili/news

No comments: