Friday, July 13, 2012

MADAKTARI KUANDAMANA TENA?

                              Dr Rodrick Kabangila upande wa kwanza kulia.
Kutokana na kusitishwa kwa ujasili wa madaktari zaidi ya 400 waliokuwepo kazini na wale wa mafunzo kwa vitendo Chama cha Madaktari (MAT) kimesema kimeandaa maandamano ya amani yatakayoshirikisha wanachama wake nchi nzima lengo likiwa ni kudai haki zao.

Katibu mkuu wa MAT Dr Rodrick Kabangila amesema tangu kuanza kwa vuguvugu la mgomo wa Madaktari, mambo mengi  yamekua yakifanywa kinyume na taaluma yao hivyo wameamua kukutana kesho ili kupanga maandamano.

Amesema lengo jingine la maandamano ya amani ni kuiomba serikali kuunda tume huru kufuatilia ishu ya kutekwa na kuteswa kwa Dr Ulimboka ambae kwa sasa yuko Afrika Kusini akipatiwa matibabu kutokana na huo mkasa pamoja na kupinga dhuluma na uonevu unaoendelea dhidi ya taaluma ya udaktari na madaktari wenyewe.

No comments: