Monday, January 21, 2013

Baada ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kumtimuwa uwanachamaMwamalala ajiunga nccr mageuzi

Edo Mwamalala, hatimaye mwanachama huyo ametangaza rasmi kujiunga na Chama cha Mageuzi ya Taifa (NCCR- Mageuzi).

Mwamalala, alisema harakati za kisiasa alizianza tangu akiwa kijana, kuwa muumini wa siasa za upinzani na rasmi alijiunga na Chadema.

Alisema ameamua kujiunga na Chama hicho kutokana na ukweli kwamba ndicho chama kinachoonekana kuwa chama chenye utu, misingi bora ya usawa, uheshimu wa haki za wanachama na Watanzania pamoja na mshikamano.

“Kwa furaha kubwa kabisa na penda kuchukua fursa hii kuwatangazia Wanambeya na umma wa Watanzania kwa kuvunja ukimya na sasa natangaza kujiunga na chama cha NCCR-Mageuzi na nisema kuwa huu ni mwanzo tu mimi nimetangulia na wengine watakuja au kufuata hatua kwa hatua”alisema Mwamalala.

Hata hivyo, Mwamalala alipinga kuwa alifukuzwa chama bali kilichotokea ni kwamba mwanzoni mwa Januari 3 mwaka huu alitangaza kujiuzulu nafasi zote za uongozi ndani ya Chadema ikiwa ni pamoja na kujivua uanachama wa chama hicho.

Pamoja na kudai kuwa hajafukuzwa, taarifa za Chama hicho zinaeleza kuwa Mwamalala alifukuzwa uwanachama tangu mwaka jana.

No comments: