Friday, January 25, 2013

MISS UTALII VIPAJI KUFANYIKA TAREHE 27.01.2012

 Tamasha kubwa la vipaji litafanyika katika Ukumbi wa Ikondolelo Lodge  Hoteli ya Kitalii  Kibamba Jumapili hii, ambapo warembo zaidi ya Thelasini   wataingia katika kuonesha vipaji mbalimbali vikiwemo na, Kucheza ngoma, Kuimba, pamoja kuonesha mavazi mbalimbali ya Asilia.

Katika Tamasha hilo Maalum Mgeni Rasmi atakuwa Muheshimiwa Iddy Azan Zungu  Mbunge wa  Jimbo la kinondoni. Sambamba na Hayo Muheshimiwa Zungu atazindua tuzo Mbalimbali za Utalii Tanzania, kama Tuzo ya Mazingira, Tuzo ya Utamaduni, Tuzo ya Jinsia, wanawake na watoto, Tuzo ya Polisi Jamii, Tuzo ya Elimu ya Jamii, Tuzo ya Hifadhi ya Serengeti, Tuzo ya Mlima Kilimanjaro, Tuzo ya Michezo pamoja na Tuzo  zengine mbalimbali.

Viingilio katika Tamasha hilo vitakuwa kama ifuatavyo, V.I.P 20,000 , Watu wa kawaida 10,000 na watoto 5,000.

Tamasha litaanza kuanzia sa nane mchana na kuendelea.

Asante.

Fredy Tony Njeje

Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano

No comments: