Thursday, January 24, 2013

RAIS KIKWETE ATEMBELEA MAKAO MAKUU YA FIFA MJINI ZURICH SWITZERLAND

 Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania, akiwa katika picha ya Pamoja na Rais wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) Joseph Sepp Blatter na Rais wa Shirikisho la Soka nchini Tanzania (TFF) Leodgar Chilla Tenga (kulia) wakati Rais Kikwete na ujumbe wake walipotembelea Makao Makuu ya FIFA mjini Zurich, Switzerland jana Januari 23, 2013 kwa Mwaliko maalum wa FIFA.
 Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania, na Rais wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) Joseph Sepp Blatter wakiwa katika mazungumzo wakati Rais Kikwete na Ujumbe wake walipotembelea Makao Makuu ya FIFA mjini Zurich, Switzerland Januari 23, 2013 kwa Mwaliko maalum wa FIFA.
  Rais wa FIFA Joseph Sepp Blatter akimkabidhi Rais Jakaya Kikwete bendera maalum ya FIFA.
Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania, akimweleza jambo Rais wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) Joseph Sepp Blatter (kulia) kuhusiana na Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Leodgar Chilla Tenga. Tenga pia ni Mwenyeketi wa  Baraza la Vyama vya Soka vya Afrika Mashariki (CECAFA).

No comments: