Monday, March 25, 2013

KAULI YA RAIS KIKWETE KUHUSU UCHAWI KWENYE SOKA LA BONGO

Moja kati ya kauli ambazo zimeingia kwenye headlines za michezo kwa wiki iliyokwisha ni kauli ya President Jakaya Kikwete, kauli kuhusu ushirikina kwenye soka la bongo aliyoitoa wakati akizindua uwanja mpya wa club ya soka ya Azam Chamazi Dar es salaam.

Namkariri akisema “najua mtapata tabu sana mkiwaleta hapa watasema kiwanja hiki kina namna, yote ni ushirikina tu…. ni wale ambao hawataki kuwekeza kwenye maendeleo ya mchezo, wanataka kuwekeza kwenye mambo ya kipuuzi… we tangu lini uchawi ukacheza mpira? ingekua uchawi unacheza mpira Afrika ingekua ina kombe la dunia na hatunyang’anywi, nyie hamjajua kwamba jambo hili la kipuuzi? mnawekeza pesa nyingi kwenye kamati ya ufundi hakuna chochote, haiwafikishi kokote”

Rais aliongeza  kwa  kusema “wekeza kwa kocha mzuri, vifaa vizuri, mafunzo mazuri, wachezaji walale mahali pazuri, Uwanja wa Azam Complex ni mzuri na wa kisasa, kuna sehemu ya mazoezi, vijana wanalala sehemu nzuri… ndio maana naamini nyinyi hakuna sababu ya kutofanikiwa"

No comments: