Saturday, March 30, 2013

"SIPO TAYARI KUJIUZULU KWA KUOGOPA MAJUNGU YA VYAMA VYA UPINZANI".....NAIBU WAZIRI WA ELIMU

Victoria fm ya mjini Mwanza jana asubuhi kipindi cha matukio wameripoti kuwa wamefanya mahojiano na naibu waziri wa elimu Bw.Philip Mulugo kuhusu tuhuma zinazomkabili ambapo amesema hawezi kujiuzulu kwa kuogopa majungu ya vyama vya upinzani wanaopika uongo juu yake ili kuwika kisiasa.

Mulugo amekanusha madai yote yaliyoandikwa na gazeti la Mwananchi na kudai kuwa kama kuna mwenye wasiwasi na elimu yake aende akamuoneshe vyeti vyake vya elimu ya sekondari hadi vya taaluma na chuo alichosoma

No comments: