Tuesday, March 12, 2013

WAKENYA WAANDAMANA KUPINGA MATOKEO YA URAIS

Polisi wa kutuliza ghasia, wamelazimika kutumia mabomu ya machozi nchini Kenya, mji wa Kisumu kuwatawanya waandamanaji waliokuwa wakipinga matokeo ya urais ambayo mgombea wao, Raila Odinga alishindwa katika uchaguzi uliofanyika nchini humo.

Vurugu hizo ziliibuka, baada ya kutangazwa kwa matokeo ya urais yaliyompa ushindi Uhuru Kenyatta.

DOKEZO
Mahakama Kuu ya Kenya ndicho chombo pekee chenye uwezo wa kutengua matokeo ya urais yaliyotangazwa IEBC.

Jopo la majaji watano ndilo litakalosikiliza rufaa ya mgombea wa Cord, Raila Odinga; nao ni Jaji Mkuu, Dk. Willy Mutunga ambaye ni Rais wa Mahakama hiyo, wengine ni Majaji Dk. Smokin Wanjala, Njoki Ndung’u, Philip Tunoi, Jackton Boma Ojwang na Mohamed Ibrahim.

Source: Mwananchi, Jumatatu, Marchi 11, 2013

No comments: