Wednesday, May 8, 2013

BALOZI WA VATICAN ALIYENUSURIKA KATIKA SHAMBULIZI LA BOMU ARUHUSIWA KUONDOKA ARUSHA

Mwakilishi wa Papa akiwa na Askofu Lebulu akitoka kwenye VIP ya Arusha Airport kuelekea kwenye ndege ya Precision .
 Ilikuwa ni dakika za majonzi na masikitiko kwa kundi lote lililokuwa limemsindikiza uwanja wa ndege Balozi wa Papa ambaye ameondoka leo mjini Arusha kuelekea Dar, baada ya kunusurika katika shambulio la bomu lililorushwa wakati akiwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi wa kanisa la Mt. Joseph Mfanyakazi huko Olasiti Arusha.

Hapa akisaidiwa na wafanyakazi wa Precision kukamilisha dokomenti zake za Usafiri, huku ulinzi ukiwa umeimarishwa
 Kwaheri Mtumishi wa Mungu, tunaomba uje tena tutakapoamua kuzindua upya Parokia Yetu ya Yosefu Mfanyakazi- Olasiti Arusha.

 Safari yako na iwe njema, Malaika wa mbinguni wakuongoze!
 Hapa anaagana na watumishi wa Mungu na kundi lote lililomsindikiza.
Tunakutakia safari njema mtumishi wa mungu hakika hila za shetani zimeshindwa na zitaendelea kushindwa kwani mungu si kipofu.

Kutoka Jamiiforum

No comments: