Thursday, May 9, 2013

SERIKALI YAPIGA MARUFUKU MIKUTANO YA DINI YENYE "VIRUSI" VYA UCHOCHEZI

Waziri wa MAmbo ya Ndani ya NChi, EMmanuel NChimbi, ameliagiza jeshi la polisi kuanzia IGP, RPC, OCD na OCS kuwachukulia hatua wale wote wanaoendesha mihadhara ya kidini yenye kuchochea vurugu na mifarakano katika jamii. ...

Nchimbi amesema kuwa kiongozi yeyote ambaye atabainika kutochukua hatua licha ya taarifa kuripotiwa kwake basi atakwenda na maji.. ...

Kauli  hiyo  ameitoa   jijini dar es salaam jana wakati akiongea na wawakilishi wa viongozi wa dini na vyombo jeshi la polisi mkoa wa dar es salaam

Waziri Nchimbi amewatahadhalisha vijana wanaoshinda kwenye mitandao na wanaotumia simu kutuma ujumbe wenye lengo la kuhamasisha chuki za kidini. Amesema kuwa kuanzia sasa serikali itachukua hatua   stahiki

Chanzo: taarifa  ya  habari ya TBC1

No comments: