Saturday, June 16, 2012

KUHUSU PREZZO KUJITOA BIG BROTHER.


Ishu ambayo imewashangaza wengi ni pale ambapo mwakilishi wa Kenya kwenye jumba la Big Brother CMB Prezzo kutangaza kwamba amechoka maisha ya kuishi kama mfungwa kwenye jumba hilo.

Mtandao wa Ghafla Kenya umeripoti kwamba hii ishu imetokea wakati Big Brother alipotangaza kupiga marufuku pombe kwa washiriki ndani ya jumba hilo, Prezzo alishikwa hasira na kusema kwamba anaweza kuondoka muda wowote, na anahisi wakati umefika.

Prezzo alimaind mpaka akawa anabishana na washiriki wenzake akiwemo Keita na kutaka mlango ufunguliwe aondoke lakini baadhi ya washiriki wenzake walimsihi asifanye hivyo.

Huu mchongo umetokea siku 30 baada ya Prezzo kuwa trending topic kwa wakenya kutokana na kuchaguliwa kwake kwenda big brother ambapo wengi walikua wanamdiss kwamba haikutakiwa apelekwe BBA.


No comments: