Friday, June 22, 2012

Mtoto Mchanga akutwa ametupwa akiwa amefariki karibu na Msikiti wa Soweto jijini Mbeya Asubuhi hii


 Katika hali ya kutatanisha wananchi wa Soweto jijini Mbeya wamekutana na Kifurushi ambacho ndani yake kulikuwa na mtoto mchanga amewekwa na kutupwa akiwa amefariki, ikiwa ni tukio la pili kutokea eneo hilo baada ya tukio kama hilo kutokea wiki mbili zilizopita.

 Hata hivyo akiongea na baadhi ya wananchi ambao hawakupenda kutaja majina yao wamedai kwamba kuna dispensary jirani hapo ambayo hawakutaka sema ni hospital ipi ambapo wana wasi wasi kwamba hutoa Mimba mabinti na kuwatupa eneo hilo. Jamani Binadamu tumekuwa wanyama huu ndio mwisho wa dunia, wanawake tunataka nini Jamani??
 Kwa picha na habari zaidi tembelea Mbeya yetu Blog

No comments: