Friday, June 22, 2012

Ureno yatua nusu fainali Euro 2012

CRISTIANO Ronaldo jana aliendelea kung’aa baada ya kufanikiwa kuiongoza nchi yake kufuzu hatua ya nusu fainali ya michuano ya Euro 2012 kwa kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Czech.
Ronaldo alifunga bao pekee kwenye mchezo huo baada ya kuiwahi krosi safi iliyopigwa na winga wa Manchester United, Luis Nani katika dakika ya 79.
Katika mchezo huo Czech walionekana kuzidiwa katika dakika zote na walifanikiwa kufika langoni mwa Ureno mara moja tu kipindi cha kwanza.
Ronaldo sasa amefikisha mabao matatu kwenye michuano hiyo baada ya kufanikiwa kufunga mawili kwenye mchezo wa makundi dhidi ya Uholanzi.
Katika historia ya Ureno haijawahi kutwaa ubingwa huu zaidi ya kufika hatua ya nusu fainali mara mbili mwaka 1984 na 2000.
Kutokana na ushindi huo, Ureno inasubiri kukutana na mshindi wa mechi kati ya Ufaransa dhidi ya Hispania katika nusu fainali ya kwanza mnamo Juni 27, 2012.

No comments: