Saturday, July 21, 2012

14 Wauawa Katika Shambulizi Marekani

                                                          Ukumbi wa Sinema mjini Denver

Rais Barack Obama na mkewe Michele wameelezea masikitiko yao kufuatia mauawaji ya watu kumi na wanne mjini denver huko colorado.

Obama alisema kuwa serikali itafanya kila juhudi kuwasaidia watu wa eneo la tukio, la Aurora wakati huu mgumu.Alikiri kuwa serikali itakahakikisha aliyehusika anakamatwa.

Mtu mmoja aliyekuwa amefunika uso wake kwa barakoa aliwauwa kwa kuwapiga risasi watu hao kumi na wanne na kuwajeruhi takriban hamsini wakati wa onyesho la filamu ya Batman,The Dark Knight Rises.

Walioshuhudia tukio hilo kwenye kitongoji cha mji huo cha Aurora walisema mtu huyo aliyekuwa amevalia kifaa cha kujikinga dhidi ya gesi aliingia ndani ya ukumbi huo na kurusha gesi ya kutoa machozi. Pindi gesi ilivyojaa kwenyen ukumbi huo mshukiwa akaanza kuwafyatulia waliokuwemo risasi.

Chanzo:http://www.bbc.co.uk/swahili/habari

No comments: