Friday, July 20, 2012

UZINDUZI WA KAMPENI YA UJENZI WA MABWENI YA WANAFUNZI WA KIKE KWA SHULE ZA SEKONDARI.

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia  na Watoto Mh.Ummy Mwalimu (MB) akicheza ‘kwaito” na wanafunzi wa shule ya sekondari ya Kibaigwa katika hafla ya uzinduzi wa kampeni ya ujenzi wa mabweni ya wanafunzi wa kike kwa shule za sekondari.
Mbunge wa viti maalumu kupitia CHADEMA Mh. Susan Lyimo(MB) akiongea katika hafla ya uzinduzi wa kampeni ya uchangiaji  ujenzi wa wa mabweni- Kibaigwa  Katika hafla hiyo jumla ya shilingi 37,214,000/= zilipatikana ikiwa ni ahadi na fedha taslim.
Dk. Naomi Katunzi  Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) akimkabidhi, Mgeni Rasmi, Naibu Waziri wa Maendeleo ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto  Mh. Ummy Mwalimu (MB) mkasi kwa ajili ya kuzindua rasmi harambee ya ujenzi wa mabweni  wanafunzi wasichana  wa shule za sekondari nchini.
Naibu Spika wa Bunge na Mbunge wa Kibaigwa Mh Job Ndugai  (MB) Akivuta utepe uliokatwa na mgeni rasmi Mh. Ummy Mwalimu huku tukio hilo likishangiliwa na wananchi wa  Kibaigwa.
Meneja wa Habari, Elimu na Mawasiliano wa Mamlaka ya Elimu Tanzania Sylvia Lupembe Gunze (kushoto) akijadiliana na Diwani wa Kibaigwa  Mh.Richard Kapinye na Afisa Elimu Taaluma  Wilaya ya Kongwa BiBI Emilia Litunguru.
Mjumbe wa Bodi ya soko la Kibaigwa, Bibi Asha Rajab akitoa ahadi ya kuchangia ujenzi wa mabweni ya shule ya Sekondari Kibaigwa. Bodi iliahidi kuchangia shilingi milioni 6 katika hafla ya uzinduzi wa kampeni ya kuchangia ujenzi wa Mabweni inayoendeshwa na TEA.
 Mgeni Rasmi Mh. Ummy Mwalimu (MB) akitoa mchango wake na akihimiza watu wengine wachangie katika Kampeni ya ujenzi wa Mambweni.
Naibu Spika wa Bunge na Mbunge wa Kongwa Mh.Job Ndugai (MB) akiongea na wananchi wa jimbo lake pamoja na wageni mbalimbali waliohudhulia uzinduzi wa kampeni ya ujenzi wa mabweni ya wanafunzi wasichana. Shule ya Sekondari Kibaigwa itafaidika na mpango huo.

No comments: