Tuesday, August 14, 2012

Serikali kujenga hospitali teule Himo

Naibu Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Aggrey Mwanri

SERIKALI imetenga kiasi sh. milioni 400 katika kipindi cha mwaka wa fedha 2012/2013 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali teule ya Wilaya kwenye Mji wa Himo.

Kauli hiyo imetolewa jana mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Aggrey Mwanri wakati akijibu swali la Mbunge wa Jimbo la Vunjo(TLP) Augustine Mrema lililouliza kuwa utekelezaji wa hospitali hiyo imefiki hutua gani? Na ni lini hospitali hiyo itakamilika.

Akijibu swali hilo Naibu Waziri huyo alisema Serikali kwa kutambua umuhimu wa mradi huo imetenga fedha hizo mbazo zitatumika kuanza ujenzi wa hospitali hiyo. Hivyo zabuni zilitangazwa na kufunguliwa Julai 18, mwaka huu na mchakato wa kumpta mkandrasi mpya unaendelea.

Naibu Waziri huyo aliongeza kuwa ni kusudio la seriklai kukamilisha ujenzi wa hospitali hii haraka iwezekanvyo ili kuwaondolea usumbufu wanananchi wa Vunjo.

Aidha Naibu Waziri huyo aliongeza kuwa Serikali iliamua kujenga hospitali ya Wilaya kwa kutenga fedha za ujenzi wa hospitali ya Himo katika mwaka wa fedha 2008/2009 kiasi cha sh. milioni 175. Fedha hizi zilikusudiwa kutumika katika ujenzi swa jingo la wagonjwa wan je (OPD) na kwa sasa jengo hilo, limekamilika na linatumika.

Aliongeza kuwa katika kipindi cha mwaka 2009/2010 Serikali ilitenga kiasi cha shilingi milioni 300, ambapo sh. milioni 200 zilitolewa na kupitia Mpango wa Ruzuku wa Serikali za Mitaa (LGDG) na sh. milioni 100 kupitia Mpango wa Maendeleo wa Afya Msingi (MMAM) kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya uchunguzi(X-ray), utawala, huduma ya mama na mtoto, vyoo, na uzio wa eneo la hospitali hiyo.

Alisema kazi hiyo alipewa mkandarasi Edcat International ConstructionLtd. Hivyo wakti utekelezaji ilidhihirika kuwa mknadarasi huyo alifanya kazi chini ya kiwango na halimashauri iliamua kuvunja mkataba wa kuzingatia kanuni na makubaliano

Katika swali lake la nyongeza Mrema aliuliza kuwa ni hatua gani zitachukuliwa dhidi ya mkandarasi huyo, ikiwemo miradi mingine iliyochini nya kiwango.

Akijibu swali hilo Naibu Waziri huyo alisema hatua iliyochukua ni kumsimamisha na pia watafanya tathimini ya fedha zilizotumika ili kungalia thamani yake, pia watatembelea miradi mingine na iliyochini ya kiwango ili kuwezackuchukua hatua.

Wakati huo huo, Serikali imepanga kununua gari la zimamoto kwa ajili ya kutoa huduma hiyo kwa majengo yenye urefu wa kufikia ghorofa 37, ambao ndio urefu wa mwisho wa gari hilo duniani katika kipindi cha mwaka wa fedha 2013/2014.

Taarifa hiyo imetolewa Agosti 13, 2012 bungeni Dodoma na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Pereira Silima wakati akijibu swali la Mbunge wa Mji Mkongwe, Muhammad Ibrahim Sanya (CUF) akitaka kujua ujenzi wa majengo mapya sasa unafikia ghorofa 20 unazidi kuongezeka ilhali hakuna vifaa vya kuweza kuzima moto kulingana na ujenzi huo.

Chanzo: www.thehabari.com

No comments: