Saturday, September 15, 2012

TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2012 LARINDIMA UWANJA WA JAMHURI MJINI DODOMA USIKU HUU


 Mkuu wa mkoa wa Dodoma Dkt. Rehema Nchimbi akitangaza namba ya mshindi wa bahati nasibu ya gari aina ya Toyota Virtz  aliyejishindia gari hilo katika droo ya tamasha la Serengeti Fiesta 2012 mkoani Dodoma kwenye tamasha la lililofanyika katika uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma usiku huu, aliyeshika kompyuta ni Meneja masoko wa kampuni ya Push Mobile Rugambo Rodney, kulia ni Mkuu wa wilaya ya Dodoma Lephy Gembe na wa pili kutoka kulia ni mwakilishi wa bodi ya michezo ya kubahatisha Bw. Humud.

Katika tamasha hilo wasanii mbalimbali wanatumbuiza katika tamasha hilo kubwa  baada ya matamasha mengine kama hayo katika mikoa ya Kilimanjaro, Tanga, Mwanza, Shinyanga, Mara, Tabora, Singida na sasa mkoani Dodoma.
Waigizaji wa filamu wakielezea uwezo wao katika kusakata muziki kutopka kulia ni Jacob Steven JB, Wema Sepetu, na Aunt Ezekikel.
Aunt Ezekiel akimwaga mauno yake lanini mbewle ya mashabiki
Raymond Kigosi Ray akifanya vitu vyake katika kusakata mayenu.
Wema Sepetu akinyonga viuono mbele ya mashabiki wa tamasha la Serengeti Fiesta uuwanja wa  mjini Jamhuri Dodoma

                                   Rachel na mmoja wa wanenguaji wake jukwaani.
 Rachel akifanya vitu vyake jukwaani
 Msanii Young Killer akionyesha uwezo wake mbele ya mashabiki kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma
 Msanii w a muziki wa kizazi kipya Bongofleva Ommy Dimpoz akifanya vitu vyake kwenye Tamasha la Serengeti Fiesta 2012 katika uwanja wa Jamhuri Mjini Dodoma
 Msanii Richa Mavoko akionyesha uwezo wake jukwaani katika tamasha la Serengeti Fiesta linalofanyika musiku huu kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.
                                            Richa Mavoko akiwaimbisha mashabiki wake

 Mtangazaji wa kituo cha rediao cha Clouds FM Gea Habib akiwa pamoja na wadau wengine wa fiesta kwenye uwanja wa jamhuri usiku huu katika tamasha la Serengeti Fiesta 2012.
                                                          Mashabiki wakiwashangilia
 Shetah msanii wa muziki wa kizazi kipya bongofleva akifanya vitu vyake jukwaani katika tamasha la Serengeti Fiesta 2012 linalofanyika usiku huu kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma,
 Msanii Diana akiwa amebebwa juu juu na wacheza shoo wake katika tamasha la Serengeti Fiesta 2012 mjini Dodoma  katika uwanja wa Jamhuri.
             Msanii Diana kutoka THT akiimba katika tamasha hilo usiku huu kwenye uwanja wa Jamhuri.

No comments: