Saturday, September 15, 2012

ZIARA YA WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA NGUDU MKOANI MWANZA

 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda  akifungua mradi ya Ufugaji nyuki katika kijiji cha  Nkalalo   wilayani kwimba akiwa katika ziara ya mkoa wa Mwanza Septemba 14, 2012. Nyuma yake ni mkewe Tunu na kushoto kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhandisi Evarest Ndikilo na Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Kwimba, Suleiman Mzee. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Wasanii wa Kikundi cha Ng’wanadelema cha Ngudu wilayni Kwimba wakicheza ngoma ya Wayeye wakai Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alipowasalimia wnanchi katika kijiji cha Nkalalo wilayani Kwimba akiwa katika ziara ya Mkoa wa Mwanza Septemba 14, 2012.
 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na mkewe Tunuwakiwa wamevikwa mavazi ya kiongozi wa jadi wa Sungusungu katika mkutano wa hadhara uliohutubiwa na Waziri Mkuu kwenye uwanja wa mpira wa miguu wa Ngudu Septemba 14, 2012.
Baadhi ya Wananchi wa Wilaya ya Kwimba  wakimsikiliza Waziri Mkuu, Mizengo Pinda wakati alipohutubia mkutano wa hadhara kwenye uwanja wa mpira wa miguu  wa Ngudu akiwa katika ziara ya mkoa wa Mwanza Septemba 14,2012. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

No comments: