Friday, October 5, 2012

Sekeseke za Mgambo wa jiji la Arusha leo na Wafanyabiashara










Katika hekaheka za safisha jiji leo arusha bado Manispal ya mjini hapa wakiendelea kuwaondoa wale wote wanaofanya biashara maeneo ya barabarani, leo nilikutana nao wakiwa wanaviondoa vibanda hivyo kwa wale waliokaidi agizo hilo.

Ni kweli jiji linakuwa safi lakini je hawa watu wanakwenda wapi? je kuondoa uwanja wa NMC waliouteuwa kuwa soko kuna eneo lingine lililoteuliwa kwa ajili yao? NMC hauna huwezo wa kuwaweka wafanyabiasha hawa je serikali wanaliona hii kama tatizo la Taifa?au hadi pochi zetu ziishe kwa kuchukuliwa na vibaka ndio wajue chazo?

Pamoja na yote tunahitaji jiji liwe safi.Basi tunawataka manispal wawe wabunifu wawatafutie mahali ambapo wataweza kujibatia riziki angalae waweze kuendesha familia zao.Je serikali inajua kuwa watoto hawaindi shule, hawapati milo mitatu kwa siku hata matibabu ndio kabisa bado kodi ya nyumba, Je Maisha bora kwa kila Mtanzania Itawezakana??????

No comments: