Monday, November 12, 2012

BALOZI KHAMIS KAGASHEKI AIPA CHANGAMOTO BODI YA UTALII TANZANIA (TTB)

 Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Khamis Kagasheki akisalimiana na Balozi wa Tanzania nchini Uingereza Balozi Peter Kallaghe, wakati alipowasili katika hafla ya chakula cha jioni katika yake, Balozi na maaofisa wa Bodi ya Utalii na Taasisi zake pamoja na maofisa wa ubalozi wa Tanzania nchini Uingereza ili kuagana na kutathimini mapungufu na mafanikio ya ushiriki wa Tanzania katika maonyesho ya dunia ya utalii World Treavel Market (WTM) yaliyomalizika mwishoni mwa wiki iliyopita nchini Uingereza, ambapo zaidi ya makampuni 55 yanayouza na kutangaza utalii wa Tanzania yalishiriki katika maonyesho hayo, maonyesho hayo hufanyika kila mwaka eneo la Excel jijini London.

Balozi Khamis Kagasheki aliitaka Bodi ya Utalii Tanzania kuongeza juhudi zaidi ili kuleta mafanikio zaidi katika maonyesho hayo na menine na kuongeza idadi ya watalii kufiki milioni moja kwa mwaka, Tanzania ikijipanga vizuri na kutangza vivutio vyake zaidi duniani inaweza kupata mafanikio zaidi katika utalii na kuongeza zaidimapato yake ikiwa ni pamoja na kukuza uchumi kupitia sekta ya utalii.
                                   Maofisa mbalimbali wakiingia katika hafla hiyo ya chakula cha jioni.
 Baadhi ya maofisa waliohudhuria katika hafla hiyo kutoka kushoto ni Dkt. Wegoro kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki Arusha , Devotha Mdachi Mkurugenzi wa Masoko wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Balozi mdogo wa Tanzania nchini Uingereza Mh. Kilumanga na Mkurugenzi wa Kituo cha Biashara cha Tanzania ubalozini Bw. Kashangwa.
                       Maofisa kutoka ubalozi wa Tanzania nchini Uingereza wakiwa katika hafla hiyo.
 Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Khamis Kagasheki kulia akimsikiliza Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Maliasili, Utalii na Ardhi wakati alipokuwa kichangia mazungumzo katika hafla ya chakula cha jioni baada ya kumalizika kwa maonyesho ya WTM nchini Uingereza mwishoni mwa wiki iliyopita, katikati ni Balozi wa Tanzania nchini humo Balozi Peter Kallaghe.
 Ofisa Habari wa TANAPA Bw. Shelutete kulia akiwa na Maofisa wa Kituo cha biashari cha Tanzania nchini Uingereza katikati ni Dilunga na kushoto ni Mohamed
  Balozi wa Tanzania nchini Uingereza Balozi Peter Kallaghe akizungumza katika hafla hiyo kulia ni Balozi Khamis Kagasheki Waziri wa Maliasili na Utalii.
 Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Khamis Kagasheki akizungumza katika hafla hiyo ambapo aliwashukuru maofisa kutoka Bodi ya Utalii na Taasisi zake pamoja na makampuni yaliyoshiriki katika maonyesho hayo kwa maandalizi mazuri katika ushiriki huo, lakini pia akaagiza kuangalia changamoto na kuzifanyia kazi ili kuboresha zaidi ushiriki wa Tanzania katika maonyesho yajayo na mengine yanayoweza kufanyika katika nchi zingine, kulia katika picha ni Balozi Peter Kallaghe na kulia ni Mama Balozi

PICHA NA WWW.FULLSHANGWEBLOG.COM

No comments: