Wednesday, January 16, 2013

JK: AZINDUA AWAMU YA KWANZA YA JENGO JIPYA LA HOSPITALI YA SHREE HINDU MANDAL JIJINI DAR ES SALAAM

 Rais Dk. Jakaya Mrisho Kikwete akiwasha mshumaa kama ishara ya uzinduzi wa Awamu ya Kwanza ya jengo jipya na Awamu ya pili ya Hospitali ya Shree Hindu Mandal ya jijini Dar es salaam leo katika Mtaa wa Nyanza, ambapo huduma hiyo itapunguza msongamano wa wagonjwa katika hospitali jijini na kuongeza wigo wa utoaji huduma n kuongeza vitanda vya kulaza wagonjwa, Hospitali ya Shree Hindu Mandalilianzishwa mwaka 1931 ikianza na Zahanati anayeshuhudiatukio hilowa pili katikati ni Mwenyekiti wa hospitali hiyo Bw Ramesh Patel.
Rais Jakaya Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Uongozi , Madaktari , Wauguzi pamoja na wafanyakazi wa hospitali ya Shree Hindu Mandal mara baada ya kuzindua rasmi leo
 Rais Dk. Jakaya Kikwete akikata utepe wakati wa uzinduzi wa hoapitali hiyo uliofanyika leo jijini Dar es salaam.


 Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mh. Raymond Mushi akizungumza na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dk. Hussein Mwinyi na Kulia ni Bw. Ramesh Patel Mwenyekiti wa Hospitali hiyo.
 Rais Jakaya Kikwete akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili hospitalini hapo kwa ajili ya kuizindua, kushoto ni Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dk. Hussein Mwinyi na Kulia ni Bw. Ramesh Patel Mwenyekiti wa Hospitali hiyo.

 Mwenyekiti wa Hospitali ya Shree Hindu Mandal Bw. Ramesh Patel akielezea historia ya hospitali hiyo.
 Rais Jakaya Kikwete akizungumza na wafanyakazi pamoja na wananchi waliohudhuria katika uzinduzi huo leo.
 Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dk. Hussein Mwinyi akimkaribisha Rais Jakaya Kikwete ili kuzungumza na wafanyakazi wa hospitali hiyo.
  Baadhi ya wauguzi na wafanyakazi wa hospitali hiyo wakiwa katika hafla ya uzinduzi huo.

 Baadhi ya wauguzi na wafanyakazi wa hospitali hiyo wakiwa katika hafla ya uzinduzi huo.

No comments: