Saturday, January 19, 2013

Mahafali ya Kidato cha Sita shule ya Sekondari Azania Mstahiki Meya Jerry Silaa akiwa mgeni rasmi

Mgeni rasmi Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa akibadilishana mawazo na baadhi ya Wanafunzi wa shule ya Sekondari Azania ambapo na yeye pia alikuwa ni miongoni mwa baadhi ya viongozi waliosoma shule hapo baada ya kuwasili kwenye hafla mahafali ya wanafunzi wa kidato cha sita.
   Picha ya chini ni  Mstahiki Meya Jerry Silaa akipunga mkono kwa wanafunzi wa shule ya sekondari Azania waliojipanga mstari kumlaki kwa furaha huku akiwa ameambatana na Mkuu wa Shule hiyo Bw. Bernard Ngoze na Makamu Mkuu wa Shule hiyo Bi. Elizabeth Ngoda (kulia).


Mgeni rasmi Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa akisalimiana na kuwapongeza baadhi ya wanafunzi wa kidato cha Sita wa Shule ya Sekondari Azania
Mstahiki Meya Jerry Silaa akipokea heshima kutoka kwa vijana wa skauti wa Shule ya Sekondari Azania

No comments: