Monday, February 4, 2013

 
  Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Dk. Jakaya Kikwete akihutubia wananchi katika sherehe za miaka 36 ya CCM zilizofanyika jioni ya leo kwenye uwanja wa Lake Tanganyika Mkoani Kigoma na kuhudhuriwa  na wananchi mbalimbali waliojitokeza kushiriki katika sherehe hizo.

Wawakilishi wa vyama rafiki vya CCM kutoka nchini Burundi CNDD kinachotawala nchini humo, na PPRD kinachotawala nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo


 Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza katika maadhimisho hayo katika uwanja wa Lake Taganyika.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdurahman Kinana akizungumza katika maadhimisho hayo.
 Msanii Diamond akiongoza kundi lake katika kutoa burudani kwa wananchi waliojitokeza katika maadhimisho hayo.
 Waziri wa Uchukuzi Dk. Harrison Mwakyembe akizungumzia mikakati ya Serikali katika maadhimisho hayo juu ya urejeshaji wa huduma za treni katika kituo cha Reli ya Kati cha Kigoma.
 Rais Jakaya Kikwete akiangalia picha zilizochorwa zikimuonesha yeye na Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius K. Nyerere wakati alipotembelea mabanda ya maonyesho katika maadhimisho ya miaka 36 ya CCM
 Rais Jakaya Kikwete akiangalia ndizi zinazozalishwa mkoani Kigoma katika banda la wakulima wa ndizi kutoka mkoa huo.


 Rais Jakaya Kikwete akiwapungia mkono wananchi wa mkoa wa Kigoma waliojitokeza kwenye maadhimisho ya miaka 36 ya CCM kwenye uwanja wa Lake Tanganyika.
Rais Jakaya Kikwete akiangalia vikundi vya ngoma mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa Lake Tanganyika kwa ajili ya kushiriki katika maadhimisho ya miaka 36 ya Chama Cha Mapinduzi CCM  Kutoka kushoto ni Makamu Mweyekiti Bara Mzee Philip Mangula, Naibu Katibu Mkuu Bara Mwigulu Nchemba na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdurahman Kinana.

No comments: