Friday, March 22, 2013

" MIMI NI MTI WENYE MATUNDA MILELE....SIOGOPI KUPIGWA MAWE"... HUU NI UJUMBE WA DIAMOND

MSANII wa muziki wa bongo fleva Diamond Platinam ameendelea kujinadi kupitia mitandao ya kijamiii huku akiteka hisia za mashabiki wake kwa kutuma baadhi ya picha zinazomuonyesha akiwa jukwaani akifanya 'makamuzi' pamoja na kutuma ujumbe wa kujipongeza kwa kazi anayoifanya

Kupitia mtandao wake wa 'Instagram' msanii huyo alituma ujumbe uliosomeka hivi "Mimi ni mti wenye matunda milele siogopi kupigwa mawe"

Ujumbe huo ulionekana kuteka baadhi ya mashabiki wake huku wengine wakituma ujumbe za kumpongeza kwa kuwa na imani hiyo huku akionyesha kutoteteleka kwa jambo lolote linalomkabili ambalo linaonyesha kutaka kumdondosha kimuziki

Maneno ya ujumbe huo pia umeonekana kutumiwa katika nyimbo yake mpya inayojulikana kwa jina la 'Muziki gani' ambayo wameshirikiana na msanii Ney wa Mitego

No comments: