Friday, May 17, 2013

Beckham astaafu soka, amfuata Sir. Ferguson

Dili la kustaafu lazidi kuitikisa nchi ya Uingereza baada ya magwiji wa soka na kocha maarufu kustaafu kufundisha soka.

 Wiki moja baada ya kustaafu kwa Sir Alex Ferguson, Paul Scholes, leo hii mchezaji wa zamani wa Man United na nahodha wa zamani wa England DAVID BECKHAM ametangaza kutundika daluga.

Beckham mwenye umri wa mika 38, ameisadia Paris Saint-Germain PSG Kutwaa mwari wa Ligue 1 nchini Ufaransa kwa mara ya kwanza ndani ya miaka 19 mwishoni mwa wiki iliyopita Pamoja na kupewa ofa ya mkataba mpya na timu hiyo ya Ufaransa, mkongwe huyo atastaafu baada ya mchezo wa mwisho tarehe 26 mwezi huu .

Alisema: “Shukrani sana kwa PSG kwa kunipa nafasi ya kuendelea kuwa hapa lakini sasa nadhani ni muda sahihi wa kustaafu, kucheza kwenye soka la kiwango cha juu”

Beckham alianza kucheza akiwa na Manchester United, akifunga mabao 85 katika mechi 394, kabla ya kuhamia Real Madrid. Aliondoka Spain kwa uhamisho mnono kujiunga na LA Galaxy mwaka 2007 pia aliwahi kucheza kwa mkopo mara kadhaa kwenye klabu ya AC Milan wakati akiwa kwenye Major League Soccer. Chanzo: Baraka Mpenja

No comments: